< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
你們要讚美耶和華! 我要在正直人的大會中,並公會中, 一心稱謝耶和華。
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
耶和華的作為本為大; 凡喜愛的都必考察。
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
他所行的是尊榮和威嚴; 他的公義存到永遠。
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
他行了奇事,使人記念; 耶和華有恩惠,有憐憫。
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
他賜糧食給敬畏他的人; 他必永遠記念他的約。
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
他向百姓顯出大能的作為, 把外邦的地賜給他們為業。
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
他手所行的是誠實公平; 他的訓詞都是確實的,
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
是永永遠遠堅定的, 是按誠實正直設立的。
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
他向百姓施行救贖, 命定他的約,直到永遠; 他的名聖而可畏。
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
敬畏耶和華是智慧的開端; 凡遵行他命令的是聰明人。 耶和華是永遠當讚美的!

< Zaburi 111 >