< Zaburi 110 >

1 Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
ダビデの歌 主はわが主に言われる、「わたしがあなたのもろもろの敵をあなたの足台とするまで、わたしの右に座せよ」と。
2 Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako.
主はあなたの力あるつえをシオンから出される。あなたはもろもろの敵のなかで治めよ。
3 Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako.
あなたの民は、あなたがその軍勢を聖なる山々に導く日に心から喜んでおのれをささげるであろう。あなたの若者は朝の胎から出る露のようにあなたに来るであろう。
4 Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”
主は誓いを立てて、み心を変えられることはない、「あなたはメルキゼデクの位にしたがってとこしえに祭司である」。
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
主はあなたの右におられて、その怒りの日に王たちを打ち破られる。
6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
主はもろもろの国のなかでさばきを行い、しかばねをもって満たし、広い地を治める首領たちを打ち破られる。
7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.
彼は道のほとりの川からくんで飲み、それによって、そのこうべをあげるであろう。

< Zaburi 110 >