< Zaburi 110 >

1 Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
לדוד מזמור נאם יהוה לאדני שב לימיני עד אשית איביך הדם לרגליך׃
2 Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako.
מטה עזך ישלח יהוה מציון רדה בקרב איביך׃
3 Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako.
עמך נדבת ביום חילך בהדרי קדש מרחם משחר לך טל ילדתיך׃
4 Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”
נשבע יהוה ולא ינחם אתה כהן לעולם על דברתי מלכי צדק׃
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
אדני על ימינך מחץ ביום אפו מלכים׃
6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
ידין בגוים מלא גויות מחץ ראש על ארץ רבה׃
7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.
מנחל בדרך ישתה על כן ירים ראש׃

< Zaburi 110 >