< Zaburi 110 >

1 Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
to/for David melody utterance LORD to/for lord my to dwell to/for right my till to set: make enemy your footstool to/for foot your
2 Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako.
tribe: rod strength your to send: depart LORD from Zion to rule in/on/with entrails: among enemy your
3 Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako.
people your voluntariness in/on/with day strength your in/on/with glory holiness from womb dawn to/for you dew youth your
4 Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”
to swear LORD and not to be sorry: relent you(m. s.) priest to/for forever: enduring upon cause Melchizedek Melchizedek
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
Lord upon right your to wound in/on/with day face: anger his king
6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
to judge in/on/with nation to fill body to wound head: leader upon land: country/planet many
7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.
from torrent: river in/on/with way: journey to drink upon so to exalt head

< Zaburi 110 >