< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
Salmo di Davide, [dato] al Capo de' Musici IO mi confido nel Signore; Come dite voi all'anima mia: Fuggite al vostro monte, [come] un uccelletto?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
Certo, ecco gli empi hanno teso l'arco, Hanno accoccate le lor saette in su la corda, Per tirar[le] contro a' diritti di cuore, in luogo scuro.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
Quando i fondamenti son ruinati, Che ha fatto il giusto?
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
Il Signore [è] nel Tempio della sua santità; Il trono del Signore [è] ne' cieli; I suoi occhi veggono, Le sue palpebre esaminano i figliuoli degli uomini.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
Il Signore esamina il giusto, e l'empio; E l'anima sua odia colui che ama la violenza.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
Egli farà piovere in su gli empi Brace, e fuoco, e solfo, E vento tempestoso, per la porzione del lor calice.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
Perciocchè il Signore [è] giusto; egli ama la giustizia; La sua faccia riguarda l'[uomo] diritto.

< Zaburi 11 >