< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
Au maître-chantre. — De David. J'ai cherché mon refuge en l'Éternel. Comment dites-vous à mon âme: «Fuis vers tes montagnes, comme l'oiseau!
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
Car voici que les méchants bandent l'arc; Ils ont ajusté leur flèche sur la corde, Pour tirer, dans l'ombre, sur ceux qui ont le coeur droit.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
Quand les fondements sont renversés, Le juste, que fera-t-il?»
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
L'Éternel est dans sa demeure sainte: L'Éternel a son trône dans les cieux. Ses yeux observent; Ses regards sondent les fils des hommes.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
L'Éternel sonde le juste; Mais il hait le méchant et celui qui se plaît à la violence.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
Il fera pleuvoir sur les méchants Des charbons ardents, du feu et du soufre. Un vent brûlant, tel est le sort qu'ils auront en partage!
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
Oui, l'Éternel est juste; il aime la justice. Les hommes droits contempleront sa face.

< Zaburi 11 >