< Zaburi 11 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
To the Overseer. — By David. In Jehovah I trusted, how say ye to my soul, 'They moved [to] Thy mountain for the bird?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
For lo, the wicked tread a bow, They have prepared their arrow on the string, To shoot in darkness at the upright in heart.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
When the foundations are destroyed, The righteous — what hath he done?
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
'Jehovah [is] in his holy temple: Jehovah — in the heavens [is] His throne. His eyes see — His eyelids try the sons of men.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
Jehovah the righteous doth try. And the wicked and the lover of violence, Hath His soul hated,
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
He poureth on the wicked snares, fire, and brimstone, And a horrible wind [is] the portion of their cup.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
For righteous [is] Jehovah, Righteousness He hath loved, The upright doth His countenance see!'