< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
to/for to conduct to/for David in/on/with LORD to seek refuge how? to say to/for soul my (to wander *Q(K)*) mountain: mount your bird
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
for behold [the] wicked to tread [emph?] bow to establish: prepare arrow their upon cord to/for to shoot in/at/by darkness to/for upright heart
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
for [the] foundation to overthrow [emph?] righteous what? to work
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
LORD in/on/with temple holiness his LORD in/on/with heaven throne his eye his to see eyelid his to test son: child man
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
LORD righteous to test and wicked and to love: lover violence to hate soul his
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
to rain upon wicked snare fire and brimstone and spirit: breath scorching portion cup their
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
for righteous LORD righteousness to love: lover upright to see face their

< Zaburi 11 >