< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
For the leader. Of David. In the Lord I take refuge. How can you tell me to flee like a bird to the mountains?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
“See! The wicked are bending the bow, their arrow is set on the string, to shoot from the shadows at the upright in heart.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
In this tearing down of foundations what good can a good person do?”
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
The Lord in his holy temple, the Lord in heaven, enthroned. His eyes watch the world, they see everyone.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
The Lord examines the righteous and wicked, and the lover of violence he hates.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
On the wicked he rains coals of fire and brimstone, and their drink will be scorching wind.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
For the Lord is just, and justice he loves; so the upright will see his face.

< Zaburi 11 >