< Zaburi 11 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
“For the leader of the music. A psalm of David.” In the LORD do I put my trust. Why say ye to me, “Flee, like a bird, to your mountain?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
For, lo! the wicked bend their bow; They make ready their arrows on the string, To shoot in secret at the upright in heart.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
If the pillars be broken down, What can the righteous do?”
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
The LORD is in his holy palace; The LORD'S throne is in heaven; His eyes behold, his eyelids prove the children of men.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
The LORD trieth the righteous; But the wicked, and the lover of violence, his soul hateth.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
Upon the wicked he will rain lightning; Fire and brimstone and a burning wind shall be the portion of their cup.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
For the LORD is righteous; he loveth righteousness; The upright shall see his face.