< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
“To the chief musician, by David.” In the Lord have I put my trust: how can ye say to my soul, Flee to your mountain as a bird?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
For lo, the wicked bend their bow, they arrange their arrow upon the string, to shoot in the dark at the upright in heart.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
For [if] the foundations be torn down, what can the righteous do?
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
The Lord is in his holy temple, the Lord hath his throne in the heavens, his eyes behold, his eyelids prove, the children of men.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
The Lord proveth the righteous; but the wicked and him that loveth violence his soul hateth.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
He letteth rain upon the wicked burning coals, fire and brimstone; and a glowing wind is the portion of their cup.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
For righteous is the Lord, he loveth righteousness: his countenance doth behold the upright.

< Zaburi 11 >