< Zaburi 11 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
For the music director: A psalm of David. Lord, you are my protection. So how can you tell me, “Fly away to the mountains like a bird”?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
Look, the wicked are drawing their bows, loading them with arrows ready to shoot from the shadows at good people.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
When the foundations of society are destroyed, what can those who live right do?
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
The Lord is in his Temple; the Lord's throne is in heaven. He keeps a close eye on everyone, watching them carefully.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
The Lord examines both those who do right and those who do evil, but he hates those who love violence.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
He will make blazing coals and sulfur rain down on the wicked; a scorching wind is what's coming on them.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
The Lord does what is right, and he loves those who live right. Those who do good will see him face to face.