< Zaburi 109 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
Müzik şefi için - Davut'un mezmuru Ey övgüler sunduğum Tanrı, Sessiz kalma!
2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
Çünkü kötüler, yalancılar Bana karşı ağzını açtı, Karalıyorlar beni.
3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
Nefret dolu sözlerle beni kuşatıp Yok yere bana savaş açtılar.
4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
Sevgime karşılık bana düşman oldular, Bense dua etmekteyim.
5 Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
İyiliğime kötülük, Sevgime nefretle karşılık verdiler.
6 Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
Kötü bir adam koy düşmanın başına, Sağında onu suçlayan biri dursun!
7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
Yargılanınca suçlu çıksın, Duası bile günah sayılsın!
8 Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
Ömrü kısa olsun, Görevini bir başkası üstlensin!
9 Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
Çocukları öksüz, Karısı dul kalsın!
10 Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
Çocukları avare gezip dilensin, Yıkık evlerinden uzakta yiyecek arasın!
11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
Bütün malları tefecinin ağına düşsün, Emeğini yabancılar yağmalasın!
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
Kimse ona sevgi göstermesin, Öksüzlerine acıyan olmasın!
13 Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
Soyu kurusun, Bir kuşak sonra adı silinsin!
14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
Atalarının suçları RAB'bin önünde anılsın, Annesinin günahı silinmesin!
15 Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
Günahları hep RAB'bin önünde dursun, RAB anılarını yok etsin yeryüzünden!
16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
Çünkü düşmanım sevgi göstermeyi düşünmedi, Ölesiye baskı yaptı mazluma, yoksula, Yüreği kırık insana.
17 Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
Sevdiği lanet başına gelsin! Madem kutsamaktan hoşlanmıyor, Uzak olsun ondan kutsamak!
18 Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
Laneti bir giysi gibi giydi, Su gibi içine, yağ gibi kemiklerine işlesin lanet!
19 Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
Bir giysi gibi onu örtünsün, Bir kuşak gibi hep onu sarsın!
20 Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
Düşmanlarıma, beni kötüleyenlere, RAB böyle karşılık versin!
21 Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
Ama sen, ey Egemen RAB, Adın uğruna bana ilgi göster; Kurtar beni, iyiliğin, sevgin uğruna!
22 Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Çünkü düşkün ve yoksulum, Yüreğim yaralı içimde.
23 Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
Batan güneş gibi geçip gidiyorum, Çekirge gibi silkilip atılıyorum.
24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
Dizlerim titriyor oruç tutmaktan; Bir deri bir kemiğe döndüm.
25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
Düşmanlarıma yüzkarası oldum; Beni görünce kafalarını sallıyorlar!
26 Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
Yardım et bana, ya RAB Tanrım; Kurtar beni sevgin uğruna!
27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
Bilsinler bu işte senin elin olduğunu, Bunu senin yaptığını, ya RAB!
28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
Varsın lanet etsin onlar, sen kutsa beni, Bana saldıranlar utanacak, Ben kulunsa sevineceğim.
29 Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
Rezilliğe bürünsün beni suçlayanlar, Kaftan giyer gibi utançlarıyla örtünsünler!
30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
RAB'be çok şükredeceğim, Kalabalığın arasında O'na övgüler dizeceğim;
31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
Çünkü O yoksulun sağında durur, Onu yargılayanlardan kurtarmak için.

< Zaburi 109 >