< Zaburi 109 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
برای سالار مغنیان. مزمور داودای خدای تسبیح من، خاموش مباش!۱
2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
زیرا که دهان شرارت ودهان فریب را بر من گشوده‌اند، و به زبان دروغ برمن سخن گفته‌اند.۲
3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
به سخنان کینه مرا احاطه کرده‌اند و بی‌سبب با من جنگ نموده‌اند.۳
4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
به عوض محبت من، با من مخالفت می‌کنند، و اما من دعا.۴
5 Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
و به عوض نیکویی به من بدی کرده‌اند. و به عوض محبت، عداوت نموده.۵
6 Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
مردی شریر را براو بگمار، و دشمن به‌دست راست او بایستد.۶
7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
هنگامی که در محاکمه بیاید، خطا کار بیرون آیدو دعای او گناه بشود.۷
8 Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
ایام عمرش کم شود ومنصب او را دیگری ضبط نماید.۸
9 Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
فرزندان اویتیم بشوند و زوجه وی بیوه گردد.۹
10 Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
و فرزندان او آواره شده، گدایی بکنند و از خرابه های خودقوت را بجویند.۱۰
11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
طلبکار تمامی مایملک او را ضبط نماید و اجنبیان محنت او را تاراج کنند.۱۱
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
کسی نباشد که بر او رحمت کند و بر یتیمان وی احدی رافت ننماید.۱۲
13 Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
ذریت وی منقطع گردند و در طبقه بعد نام ایشان محو شود.۱۳
14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
عصیان پدرانش نزد خداوند به یاد آورده شودو گناه مادرش محو نگردد.۱۴
15 Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
و آنها در مد نظرخداوند دائم بماند تا یادگاری ایشان را از زمین ببرد.۱۵
16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
زیرا که رحمت نمودن را به یاد نیاورد، بلکه بر فقیر و مسکین جفا کرد و بر شکسته دل تااو را به قتل رساند.۱۶
17 Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
چون که لعنت را دوست می‌داشت بدو رسیده و چون که برکت رانمی خواست، از او دور شده است.۱۷
18 Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
و لعنت رامثل ردای خود در بر‌گرفت و مثل آب به شکمش درآمد و مثل روغن در استخوانهای وی.۱۸
19 Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
پس مثل جامه‌ای که او را می‌پوشاند، و چون کمربندی که به آن همیشه بسته می‌شود، خواهدبود.۱۹
20 Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
این است اجرت مخالفانم از جانب خداوند و برای آنانی که بر جان من بدی می‌گویند.۲۰
21 Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
اما تو‌ای یهوه خداوند به‌خاطر نام خود بامن عمل نما؛ چون که رحمت تو نیکوست، مراخلاصی ده.۲۱
22 Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
زیرا که من فقیر و مسکین هستم ودل من در اندرونم مجروح است.۲۲
23 Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
مثل سایه‌ای که در زوال باشد رفته‌ام و مثل ملخ رانده شده‌ام.۲۳
24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
زانوهایم از روزه داشتن می‌لرزد و گوشتم ازفربهی کاهیده می‌شود.۲۴
25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
و من نزد ایشان عارگردیده‌ام. چون مرا می‌بینند سر خود رامی جنبانند.۲۵
26 Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
‌ای یهوه خدای من مرا اعانت فرما، و به حسب رحمت خود مرا نجات ده،۲۶
27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
تا بدانند که این است دست تو، و تو‌ای خداوند این را کرده‌ای.۲۷
28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
ایشان لعنت بکنند، اما تو برکت بده. ایشان برخیزند و خجل گردند و اما بنده توشادمان شود.۲۸
29 Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
جفا کنندگانم به رسوایی ملبس شوند و خجالت خویش را مثل ردا بپوشند.۲۹
30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
خداوند را به زبان خود بسیار تشکر خواهم کرد و او را در جماعت کثیر حمد خواهم گفت.۳۰
31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
زیرا که به‌دست راست مسکین خواهد ایستادتا او را از آنانی که بر جان او فتوا می‌دهندبرهاند.۳۱

< Zaburi 109 >