< Zaburi 109 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
聖歌隊の指揮者によってうたわせたダビデの歌 わたしのほめたたえる神よ、もださないでください。
2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
彼らは悪しき口と欺きの口をあけて、わたしにむかい、偽りの舌をもってわたしに語り、
3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
恨みの言葉をもってわたしを囲み、ゆえなくわたしを攻めるのです。
4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
彼らはわが愛にむくいて、わたしを非難します。しかしわたしは彼らのために祈ります。
5 Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
彼らは悪をもってわが善に報い、恨みをもってわが愛に報いるのです。
6 Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
彼の上に悪しき人を立て、訴える者に彼を訴えさせてください。
7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
彼がさばかれるとき、彼を罪ある者とし、その祈を罪に変えてください。
8 Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
その日を少なくし、その財産をほかの人にとらせ、
9 Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
その子らをみなしごにし、その妻をやもめにしてください。
10 Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
その子らを放浪者として施しをこわせ、その荒れたすまいから追い出させてください。
11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
彼が持っているすべての物を債主に奪わせ、その勤労の実をほかの人にかすめさせてください。
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
彼にいつくしみを施す者はひとりもなく、またそのみなしごをあわれむ者もなく、
13 Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
その子孫を絶えさせ、その名を次の代に消し去ってください。
14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
その父たちの不義は主のみ前に覚えられ、その母の罪を消し去らないでください。
15 Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
それらを常に主のみ前に置き、彼の記憶を地から断ってください。
16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
これは彼がいつくしみを施すことを思わず、かえって貧しい者、乏しい者を責め、心の痛める者を殺そうとしたからです。
17 Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
彼はのろうことを好んだ。のろいを彼に臨ませてください。彼は恵むことを喜ばなかった。恵みを彼から遠ざけてください。
18 Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
彼はのろいを衣のように着た。のろいを水のようにその身にしみこませ、油のようにその骨にしみこませてください。
19 Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
またそれを自分の着る着物のようにならせ、常に締める帯のようにならせてください。
20 Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
これがわたしを非難する者と、わたしに逆らって悪いことを言う者の主からうける報いとしてください。
21 Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
しかし、わが主なる神よ、あなたはみ名のために、わたしを顧みてください。あなたのいつくしみの深きにより、わたしをお助けください。
22 Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
わたしは貧しく、かつ乏しいのです。わたしの心はわがうちに傷ついています。
23 Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
わたしは夕日の影のように去りゆき、いなごのように追い払われます。
24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
わたしのひざは断食によってよろめき、わたしの肉はやせ衰え、
25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
わたしは彼らにそしられる者となりました。彼らはわたしを見ると、頭を振ります。
26 Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
わが神、主よ、わたしをお助けください。あなたのいつくしみにしたがって、わたしをお救いください。
27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
主よ、これがあなたのみ手のわざであること、あなたがそれをなされたことを、彼らに知らせてください。
28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
彼らはのろうけれども、あなたは祝福されます。わたしを攻める者をはずかしめ、あなたのしもべを喜ばせてください。
29 Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
わたしを非難する者にはずかしめを着せ、おのが恥を上着のようにまとわせてください。
30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
わたしはわが口をもって大いに主に感謝し、多くの人のなかで主をほめたたえます。
31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
主は貧しい者の右に立って、死罪にさだめようとする者から彼を救われるからです。