< Zaburi 109 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
Voor muziekbegeleiding. Een psalm van David. Mijn God, tot wien mijn loflied klinkt, Zwijg toch niet stil!
2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
Want men zet een mond vol boosheid en bedrog tegen mij op, En belastert mij met leugentongen;
3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
Men bestookt mij met woorden van haat, En bestrijdt mij zonder enige grond;
4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
Men belaagt mij tot loon voor mijn liefde, En tot loon voor mijn bidden;
5 Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
Men vergeldt mij kwaad voor goed, En haat voor mijn liefde.
6 Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
Stel een gewetenloos rechter over hem aan, En aan zijn rechterhand trede een valse aanklager op;
7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
Voor het gerecht worde hij schuldig bevonden, En smeke hij tevergeefs om genade.
8 Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
Mogen zijn dagen maar kort zijn, En zijn ambt aan een ander vervallen.
9 Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
Zijn kinderen mogen wezen, Zijn vrouw een weduwe worden;
10 Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
Mogen zijn zonen als bedelaars zwerven, Zelfs uit hun krotten worden verjaagd.
11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
De woekeraar legge beslag op heel zijn bezit, En vreemden mogen met zijn verdiensten gaan strijken.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
Laat niemand zich zijner ontfermen, Niemand zich over zijn wezen erbarmen;
13 Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
Laat zijn kroost ten ondergang worden gedoemd, Zijn naam al verdwijnen in het eerste geslacht.
14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
Moge Jahweh de misdaad zijner vaderen gedenken, En de schuld van zijn moeder nooit worden gedelgd;
15 Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
Jahweh houde ze altijd voor ogen, Zodat zelfs hun aandenken van de aarde verdwijnt.
16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
Want hij dacht er niet aan, barmhartig te zijn, Maar vervolgde den ellendige, arme en bedroefde ten dode.
17 Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
Hij hield van vervloeking: die treffe hem dan; Geen zegen wilde hij spreken: die blijve hem verre!
18 Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
De vloek trok hij aan als een kleed: Die dringe hem als water in het lijf, als olie in zijn gebeente;
19 Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
Die worde de mantel, waarin hij zich hult, De gordel, die hij altijd moet dragen.
20 Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
Zó moge Jahweh mijn haters vergelden, En die laag van mij lasteren!
21 Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
Maar treed Gìj voor mij op, o Jahweh, mijn Heer, En red mij omwille van uw Naam naar de rijkdom uwer genade!
22 Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Want ik ben arm en ellendig, En mijn hart krimpt ineen in mijn borst;
23 Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
Ik zink weg als een verdwijnende schaduw, Word voortgejaagd als een sprinkhanenzwerm;
24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
Van het vasten knikken mijn knieën, En mijn vermagerd lichaam schrompelt ineen.
25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
Zó ben ik hun een bespotting geworden; Die mij zien, schudden meewarig het hoofd.
26 Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
Help mij, Jahweh, mijn God, En red mij naar uw genade;
27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
Opdat men erkenne, dat het uw hand is, Jahweh: dat Gij het volbracht!
28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
Laat hèn dan maar vloeken, als Gìj mij wilt zegenen; Mijn vijand zich schamen, maar uw knecht zich verheugen;
29 Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
Mogen mijn tegenstanders met smaad worden bekleed, En zich in hun schande hullen als in een mantel!
30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
Dan zal ik Jahweh juichend danken, En voor een talloze schare Hem prijzen;
31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
Omdat Hij aan de rechterhand van den ongelukkige staat, Om hem te redden, van die hem verdoemen!

< Zaburi 109 >