< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Una canción. Un Salmo de David. Mi corazón está firme, Dios. Cantaré y haré música con mi alma.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
¡Despertad, arpa y lira! Despertaré al amanecer.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Te daré gracias, Yahvé, entre las naciones. Te cantaré alabanzas entre los pueblos.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
Porque tu bondad es grande sobre los cielos. Tu fidelidad llega a los cielos.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
¡Sé exaltado, Dios, por encima de los cielos! Que tu gloria sea sobre toda la tierra.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Para que tu amado sea liberado, salva con tu mano derecha, y respóndenos.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Dios ha hablado desde su santuario: “En triunfo, Dividiré Siquem, y mediré el valle de Sucot.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Galaad es mía. Manasés es mío. Efraín también es mi casco. Judá es mi cetro.
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab es mi lavadero. Lanzaré mi sandalia sobre Edom. Gritaré sobre Filistea”.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
¿Quién me llevará a la ciudad fortificada? ¿Quién me llevará a Edom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
¿No nos has rechazado, Dios? No sales, Dios, con nuestros ejércitos.
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Danos ayuda contra el enemigo, porque la ayuda del hombre es vana.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
A través de Dios, nosotroslo haremos con valentía, ya que es él quien va a pisotear a nuestros enemigos.

< Zaburi 108 >