< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Песнь. Псалом Давида. Готово сердце мое, Боже, готово сердце мое; буду петь и воспевать во славе моей.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Воспрянь, псалтирь и гусли! Я встану рано.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Буду славить Тебя, Господи, между народами; буду воспевать Тебя среди племен,
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
ибо превыше небес милость Твоя и до облаков истина Твоя.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Будь превознесен выше небес, Боже; над всею землею да будет слава Твоя,
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
дабы избавились возлюбленные Твои: спаси десницею Твоею и услышь меня.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Бог сказал во святилище Своем: “восторжествую, разделю Сихем и долину Сокхоф размерю;
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Мой Галаад, Мой Манассия, Ефрем - крепость главы Моей, Иуда - скипетр Мой,
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Моав - умывальная чаша Моя, на Едома простру сапог Мой, над землею Филистимскою восклицать буду”.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Кто введет меня в укрепленный город? Кто доведет меня до Едома?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Не Ты ли, Боже, Который отринул нас и не выходишь, Боже, с войсками нашими?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Подай нам помощь в тесноте, ибо защита человеческая суетна.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
С Богом мы окажем силу: Он низложит врагов наших

< Zaburi 108 >