< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
[Ein Lied, ein Psalm. [Eig. Ein Psalm-Lied] Von David.] Befestigt [O. Fest; vergl. Ps. 57,7-11] ist mein Herz, o Gott! ich will singen und Psalmen singen; auch meine Seele. [S. die Anm. zu Ps. 16,9]
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Wachet auf, Harfe und Laute! ich will aufwecken die Morgenröte.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Ich will dich preisen unter den Völkern, Jehova, und dich besingen unter den Völkerschaften;
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
Denn groß ist deine Güte über die Himmel hinaus, und bis zu den Wolken deine Wahrheit.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Erhebe dich über die Himmel, o Gott! und über der ganzen Erde sei deine Herrlichkeit!
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Damit [Vergl. Ps. 60,5-12] befreit werden deine Geliebten, rette durch deine Rechte und erhöre uns!
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Gott hat geredet in seiner Heiligkeit: Frohlocken will ich, will Sichem verteilen, und das Tal Sukkoth ausmessen.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Mein ist Gilead, mein Manasse, und Ephraim ist die Wehr meines Hauptes, Juda mein Herrscherstab. [And. üb.: Gesetzgeber]
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab ist mein Waschbecken; auf Edom will ich meine Sandale werfen, über Philistäa will ich jauchzen.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Wer wird mich führen in die befestigte Stadt, wer wird mich leiten bis nach Edom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Nicht du, Gott, der du uns verworfen hast und nicht auszogest, o Gott, mit unseren Heeren?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Schaffe uns Hülfe aus der Bedrängnis! [O. vom Bedränger] Menschenrettung ist ja eitel.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Mit Gott werden wir mächtige Taten [Eig. Mächtiges] tun; und er, er wird unsere Bedränger zertreten.

< Zaburi 108 >