< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Cantique et psaume de David. Mon cœur est prêt, ô Dieu, mon cœur est prêt; je vais chanter des psaumes en ma gloire.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Réveillez-vous, ma harpe et ma cithare; je me lèverai dès l'aurore.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Seigneur, je te rendrai gloire parmi les peuples; je te chanterai des psaumes parmi les Gentils.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
Car ta miséricorde est plus grande que les cieux; et ta vérité va jusqu'aux nues.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Dieu, sois exalté au-dessus des cieux; que ta gloire soit répandue sur toute la terre!
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Afin que tes bien-aimés soient délivrés, sauve-moi par ta droite, et exauce-moi.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Dieu a parlé dans son sanctuaire; je me réjouirai, et je partagerai Sichem, et je mesurerai le val des Tabernacles.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
A moi est Galaad, à moi Manassé; Ephraïm est l'appui de ma tête; Juda est mon roi,
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Et Moab le vase de mon espérance. Je poserai ma sandale sur l'Idumée, les étrangers me sont soumis.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Qui me ramènera dans la ville forte? Qui me guidera jusqu'à la terre d'Édom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
N'est-ce pas toi, ô Dieu, qui nous avais repoussés; ô Dieu, toi qui ne sortais plus à la tête de nos armées?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Donne-nous ton secours pour nous tirer de la tribulation; car il est vain, le salut qui vient de l'homme.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
En Dieu nous mettons notre force, et lui-même réduira à néant nos ennemis.

< Zaburi 108 >