< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
The song of `the salm of Dauid. Min herte is redi, God, myn herte is redi; Y schal singe, and Y schal seie salm in my glorie.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
My glorie, ryse thou vp, sautrie and harp, rise thou vp; Y schal rise vp eerli.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Lord, Y schal knouleche to thee among puplis; and Y schal seie salm to thee among naciouns.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
For whi, God, thi merci is greet on heuenes; and thi treuthe is til to the cloudis.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
God, be thou enhaunsid aboue heuenes; and thi glorie ouer al erthe.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
That thi derlingis be delyuerid, make thou saaf with thi riythond, and here me; God spak in his hooli.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
I schal make ful out ioye, and Y schal departe Siccimam; and Y schal mete the grete valei of tabernaclis.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Galaad is myn, and Manasses is myn; and Effraym is the vptaking of myn heed. Juda is my king; Moab is the caudron of myn hope.
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
In to Ydume Y schal stretche forth my scho; aliens ben maad frendis to me.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Who schal lede me forth in to a stronge citee; who schal lede me forth til in to Idume?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Whether not thou, God, that hast put vs awei; and, God, schalt thou not go out in oure vertues?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Yyue thou help to vs of tribulacioun; for the heelthe of man is veyn.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
We schulen make vertu in God; and he schal bringe oure enemyes to nouyt.

< Zaburi 108 >