< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
song melody to/for David to establish: establish heart my God to sing and to sing also glory my
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
to rouse [emph?] [the] harp and lyre to rouse dawn
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
to give thanks you in/on/with people LORD and to sing you not people
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
for great: large from upon heaven kindness your and till cloud truth: faithful your
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
to exalt [emph?] upon heaven God and upon all [the] land: country/planet glory your
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
because to rescue [emph?] beloved your to save [emph?] right your and to answer me
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
God to speak: promise in/on/with holiness his to exult to divide Shechem and valley Succoth to measure
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
to/for me Gilead to/for me Manasseh and Ephraim security head: leader my Judah to decree me
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab pot washing my upon Edom to throw sandal my upon Philistia to shout
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
who? to conduct me city fortification who? to lead me till Edom
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
not God to reject us and not to come out: come God in/on/with army our
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
to give [emph?] to/for us help from enemy and vanity: vain deliverance: salvation man
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
in/on/with God to make: do strength and he/she/it to trample enemy our

< Zaburi 108 >