< Zaburi 108 >
1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
“A song or psalm of David.” My heart is firm, O God; I will sing and give praise, even with my spirit.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Awake, psaltery and harp: I will wake up the morning-dawn.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will give thee thanks among the people, O Lord: and I will sing praises unto thee among the nations.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
For great above the heavens is thy kindness, and thy truth reacheth even unto the skies.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Exalt thyself above the heavens, O God; and above all the earth thy glory.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
In order that thy beloved may be delivered: help with thy right hand, and answer me.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
God hath spoken in his holiness: I will exult, I will divide Shechem, and the valley of Succoth will I measure out.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Mine id Gil'ad, and mine is Menasseh; Ephraim also is the strong-hold of my head; of Judah are my chiefs.
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab is my washpot; upon Edom will I cast my shoe; over Philistia will I triumph.
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Who will bring me into the fortified city? who will lead me as far as Edom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Behold, it is thou, O God, who hast cast us off; and thou, O God, goest not forth with our armies.
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Give us help against the assailant; for vain is the help of man.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Through God shall we do valiantly; for he it is that will tread down our adversaries.