< Zaburi 108 >
1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
A song. A Psalm of David. My heart is steadfast, O God; I will sing and make music with all my being.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Awake, O harp and lyre! I will awaken the dawn.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will praise You, O LORD, among the nations; I will sing Your praises among the peoples.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
For Your loving devotion extends beyond the heavens, and Your faithfulness reaches to the clouds.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Be exalted, O God, above the heavens; may Your glory cover all the earth.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Respond and save us with Your right hand, that Your beloved may be delivered.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
God has spoken from His sanctuary: “I will triumph! I will parcel out Shechem and apportion the Valley of Succoth.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Gilead is Mine, and Manasseh is Mine; Ephraim is My helmet, Judah is My scepter.
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab is My washbasin; upon Edom I toss My sandal; over Philistia I shout in triumph.”
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Who will bring me to the fortified city? Who will lead me to Edom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Have You not rejected us, O God? Will You no longer march out, O God, with our armies?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Give us aid against the enemy, for the help of man is worthless.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
With God we will perform with valor, and He will trample our enemies.