< Zaburi 108 >
1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Pjesma. Psalam. Davidov. Moje je srce sigurno, Bože, sigurno je srce moje: pjevat ću i svirati.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Probudi se, dušo moja! Probudi se, harfo i citaro! Probudit ću zoru jutarnju.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Hvalit ću te, Jahve, među narodima, među pucima tebi ću pjevati,
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
jer do neba je dobrota tvoja, do oblaka tvoja vjernost.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Uzvisi se, Bože, nad nebesa, slava tvoja nek' je nad svom zemljom!
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Da ti se ljubimci izbave, desnicom pomozi, usliši nas!
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Bog reče u svom Svetištu: “Šekem ću razdijelit' kličući, dolinu ću Sukot izmjeriti.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Moj je Gilead, moj Manaše, Efrajim mi kaciga, Judeja žezlo moje!
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab je sud iz kojeg se umivam, na Edom ću baciti obuću, nad Filistejcem slaviti pobjedu!”
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Tko će me dovesti do utvrđena grada, tko će me dovesti do Edoma?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Zar nećeš ti, o Bože, što nas odbaci? Zar nećeš više, Bože, sa četama našim?
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Pomozi nam protiv dušmana, jer je ljudska pomoć ništavna!
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
S Božjom pomoću hrabro ćemo se boriti, Bog će zgaziti naše dušmane.