< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
¡Den gracias a Yavé, Porque Él es bueno, Porque para siempre es su misericordia!
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Que lo digan los redimidos de Yavé, Los que redimió del poder del adversario,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Y los que congregó de las tierras, Del oriente y del occidente, del norte y del sur.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Ellos vagaron en un desierto, en región despoblada. No hallaron un camino hacia una ciudad habitada.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Tenían hambre y sed. Sus almas desfallecían en ellos.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Pero clamaron a Yavé en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Los condujo por un camino recto Para ir a una ciudad habitada.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Porque Él sacia al alma que tiene sed Y llena de bien al alma que tiene hambre.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Vivían en oscuridad y sombra de muerte, Prisioneros en aflicción y cadenas,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Por cuanto fueron rebeldes a las Palabras de ʼEL Y trataron con desprecio el consejo del ʼElyón.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Por tanto Él quebrantó sus corazones con trabajo. Cayeron y no hubo quien los ayudara.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Pero en su angustia clamaron a Yavé, Él los libró de sus aflicciones.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Los sacó de la oscuridad y de la sombra de muerte, Y rompió sus ataduras.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Porque quebró las puertas de bronce, Y desmenuzó los cerrojos de hierro.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fueron afligidos los necios a causa de su camino rebelde, Y a causa de sus iniquidades fueron afligidos.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Su vida aborreció toda clase de alimento, Y se acercaron a las puertas de la muerte.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Pero a Yavé clamaron en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Envió su Palabra y los sanó, Y [los] libró de sus destrucciones.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Ofrezcan también sacrificios de acción de gracias Y proclamen sus obras con júbilo.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Los que bajan en naves al mar, Los cuales hacen negocios sobre inmensas aguas.
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Ellos vieron las obras de Yavé Y sus maravillas en las profundidades.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Porque Él habló y levantó un viento tempestuoso Que levantó las olas del mar.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Subían hacia los cielos, Bajaban a las profundidades, Su alma se derretía en su desesperación.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Temblaban y se tambaleaban como ebrios, Y toda su pericia fue inútil.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
En su angustia clamaron a Yavé, Y Él los sacó de sus angustias.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Calmó la tormenta De tal modo que sus olas se apaciguaron.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Entonces se alegraron porque se calmaron. Y así los guía al puerto que anhelan.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Exáltenlo en la congregación del pueblo, Y alábenlo en la reunión de los ancianos.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Él cambia ríos en desierto Y manantiales de aguas en sequedales,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
La tierra fructífera en estéril, Por la perversidad de los que viven en ella.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Él convierte el desierto en estanques de aguas, Y la tierra seca en manantiales.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Allí coloca a los que tienen hambre, Para que establezcan una ciudad habitada.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Siembran campos y plantan viñas Y recogen abundante fruto.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Los bendice, Y se multiplican grandemente. No permite que disminuya su ganado
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Cuando son menguados y abatidos Por medio de opresión, aflicción y tristeza.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Él derrama menosprecio sobre los nobles, Y los destina a vagar errantes en un desierto.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Pero Él pone en alto a los pobres lejos de la aflicción Y hace que [sus] familias sean como un rebaño.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Los rectos lo ven y se alegran, Pero toda injusticia cierra su boca.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
¿Quién es sabio? Observe estas cosas, Y entenderá las misericordias de Yavé.