< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Celebrad a Yahvé porque es bueno, porque su misericordia permanece para siempre.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Así digan los rescatados de Yahvé, los que Él redimió de manos del enemigo,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
y a quienes Él ha congregado de las tierras del Oriente y del Occidente, del Norte y del Mediodía.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Erraban por el desierto, en la soledad, sin hallar camino a una ciudad donde morar.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Sufrían hambre y sed; su alma desfallecía en ellos.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Y clamaron a Yahvé en su angustia, y Él los sacó de sus tribulaciones.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Y los condujo por camino derecho, para que llegasen a una ciudad donde habitar.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Den gracias a Yahvé por su misericordia, y por sus maravillas en favor de los hijos de los hombres.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Porque sació al alma sedienta, y a la hambrienta colmó de bienes.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Moraban en tinieblas y sombras, cautivos de la miseria y del hierro;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
porque habían resistido a las palabras de Dios y despreciado el consejo del Altísimo.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Y Él humilló su corazón con trabajos; sucumbían y no había quien los socorriese.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Y clamaron a Yahvé en su angustia, y Él los sacó de sus tribulaciones.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Y los libró de las tinieblas y de las sombras, y rompió sus cadenas.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Den gracias a Yahvé por su misericordia, y por sus maravillas en favor de los hijos de los hombres;
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
porque Él rompió las puertas de bronce, e hizo pedazos los cerrojos de hierro.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Estaban enfermos a causa de su iniquidad, y afligidos a causa de sus delitos;
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
sintieron náuseas de todo alimento, y llegaron a las puertas de la muerte.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Y clamaron a Yahvé en su angustia, y Él los sacó de sus tribulaciones.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Envió su Palabra para sanarlos y arrancarlos de la perdición.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Den gracias a Yahvé por su misericordia, y por sus maravillas en favor de los hijos de los hombres,
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
y ofrezcan sacrificios de alabanza, y publiquen con júbilo sus obras.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Surcaban en naves el mar, traficando sobre las vastas ondas,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
esos vieron las obras del Señor, y sus maravillas en el piélago.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Con Su palabra suscitó un viento borrascoso, que levantó las olas del mar;
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
subían hasta el cielo y descendían hasta el abismo, su alma desmayaba en medio de sus males.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Titubeaban y se tambaleaban como ebrios, y les fallaba toda su pericia.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Y clamaron a Yahvé en su angustia, y Él los sacó de sus tribulaciones.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Tornó el huracán en suave brisa, y las ondas del mar callaron.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Y se alegraron de que callasen, y los condujo al puerto deseado.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Den gracias a Yahvé por su misericordia, y por sus maravillas en favor de los hijos de los hombres.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Celébrenlo en la asamblea del pueblo, y en la reunión de los ancianos, cántenle.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Él convirtió los ríos en desierto, y los manantiales en árida tierra,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
el suelo fructífero en un salobral, por la malicia de sus moradores.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Él mismo ha convertido el desierto en lago y la tierra árida en manantiales,
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
allí coloca a los hambrientos, y fundan una ciudad para habitarla.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Siembran los campos y plantan viñas, y obtienen de ellos los frutos.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Bendecidos por Él se multiplican en gran manera, y sus ganados no disminuyen nunca.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Aunque reducidos a pocos y despreciados, por el peso del infortunio y de la aflicción,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Aquel que derrama desprecio sobre los príncipes, y los hace errar por desiertos sin huellas,
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
ha levantado de la miseria al indigente, y hace las familias numerosas como rebaños.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Lo ven los justos y se alegran, y toda malicia cierra su boca.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
¿Quién es el sabio que considere estas cosas y comprenda las misericordias del Señor?