< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Louvae ao Senhor, porque elle é bom, porque a sua benignidade dura para sempre.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Digam-n'o os remidos do Senhor, os que remiu da mão do inimigo,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
E os que congregou das terras do oriente e do occidente, do norte e do sul.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Andaram desgarrados pelo deserto, por caminhos solitarios; não acharam cidade para habitarem.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Famintos e sedentos, a sua alma n'elles desfallecia.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
E clamaram ao Senhor na sua angustia, e os livrou das suas necessidades.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
E os levou por caminho direito, para irem a uma cidade de habitação.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Pois fartou a alma sedenta, e encheu de bondade a alma faminta.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Tal como a que se assenta nas trevas e sombra da morte, presa em afflicção e em ferro;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Porquanto se rebellaram contra as palavras de Deus, e desprezaram o conselho do Altissimo,
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Portanto lhes abateu o coração com trabalho; tropeçaram, e não houve quem os ajudasse.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Então clamaram ao Senhor na sua angustia, e os livrou das suas necessidades.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Tirou-os das trevas e sombra da morte; e quebrou as suas prisões.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Pois quebrou as portas de bronze; e despedaçou os ferrolhos de ferro.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Os loucos, por causa da sua transgressão, e por causa das suas iniquidades, são afflictos.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
A sua alma aborreceu toda a comida, e chegaram até ás portas da morte.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Então clamaram ao Senhor na sua angustia: e elle os livrou das suas necessidades.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Enviou a sua palavra, e os sarou; e os livrou da sua destruição.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
E offereçam os sacrificios de louvor, e relatem as suas obras com regozijo.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Os que descem ao mar em navios, mercando nas grandes aguas,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Esses vêem as obras do Senhor, e as suas maravilhas no profundo.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Pois elle manda, e se levanta o vento tempestuoso, que eleva as suas ondas.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Sobem aos céus; descem aos abysmos, e a sua alma se derrete em angustias.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Andam e cambaleam como ebrios, e perderam todo o tino.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Então clamam ao Senhor na sua angustia; e elle os livra das suas necessidades.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Faz cessar a tormenta, e calam-se as suas ondas.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Então se alegram, porque se aquietaram; assim os leva ao seu porto desejado.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Exaltem-n'o na congregação do povo, e glorifiquem-n'o na assembléa dos anciãos.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Elle converte os rios em um deserto, e as fontes em terra sedenta:
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A terra fructifera em esteril, pela maldade dos que n'ella habitam.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Converte o deserto em lagoa, e a terra secca em fontes.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
E faz habitar ali os famintos, para que edifiquem cidade para habitação;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
E semeiam os campos e plantam vinhas, que produzem fructo abundante.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Tambem os abençoa, de modo que se multiplicam muito; e o seu gado não diminue.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Depois se diminuem e se abatem, pela oppressão, afflicção e tristeza.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Derrama o desprezo sobre os principes, e os faz andar desgarrados pelo deserto, onde não ha caminho.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Porém livra ao necessitado da oppressão em um logar alto, e multiplica as familias como rebanhos.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Os rectos o verão, e se alegrarão, e toda a iniquidade tapará a bocca.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Quem é sabio observará estas coisas, e elles comprehenderão as benignidades do Senhor.