< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Alleluia alleluia. Confitemini Domino quoniam bonus: quoniam in saeculum misericordia eius.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Dicant qui redempti sunt a Domino, quos redemit de manu inimici: et de regionibus congregavit eos:
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
A solis ortu, et occasu: ab aquilone, et mari.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Erraverunt in solitudine in inaquoso: viam civitatis habitaculi non invenerunt,
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Esurientes, et sitientes: anima eorum in ipsis defecit.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum eripuit eos.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Et deduxit eos in viam rectam: ut irent in civitatem habitationis.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Quia satiavit animam inanem: et animam esurientem satiavit bonis.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Sedentes in tenebris, et umbra mortis: vinctos in mendicitate, et ferro.
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Quia exacerbaverunt eloquia Dei: et consilium Altissimi irritaverunt.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Et humiliatum est in laboribus cor eorum: infirmati sunt, nec fuit qui adiuvaret.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Et eduxit eos de tenebris, et umbra mortis: et vincula eorum dirupit.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Quia contrivit portas aereas: et vectes ferreos confregit.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Suscepit eos de via iniquitatis eorum: propter iniustitias enim suas humiliati sunt.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Omnem escam abominata est anima eorum: et appropinquaverunt usque ad portas mortis.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Misit verbum suum, et sanavit eos: et eripuit eos de interitionibus eorum.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Et sacrificent sacrificium laudis: et annuncient opera eius in exultatione.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Qui descendunt mare in navibus, facientes operationem in aquis multis.
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Ipsi viderunt opera Domini, et mirabilia eius in profundo.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Dixit, et stetit spiritus procellae: et exaltati sunt fluctus eius.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Ascendunt usque ad caelos, et descendunt usque ad abyssos: anima eorum in malis tabescebat.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Turbati sunt, et moti sunt sicut ebrius: et omnis sapientia eorum devorata est.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur, et de necessitatibus eorum eduxit eos.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Et statuit procellam eius in auram: et siluerunt fluctus eius.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Et laetati sunt quia siluerunt: et deduxit eos in portum voluntatis eorum.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Et exaltent eum in ecclesia plebis: et in cathedra seniorum laudent eum.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Posuit flumina in desertum: et exitus aquarum in sitim.
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Terram fructiferam in salsuginem, a malitia inhabitantium in ea.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Posuit desertum in stagna aquarum: et terram sine aqua in exitus aquarum.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Et collocavit illic esurientes: et constituerunt civitatem habitationis.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Et seminaverunt agros, et plantaverunt vineas: et fecerunt fructum nativitatis.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Et benedixit eis, et multiplicati sunt nimis: et iumenta eorum non minoravit.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Et pauci facti sunt: et vexati sunt a tribulatione malorum, et dolore.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Effusa est contentio super principes: et errare fecit eos in invio, et non in via.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Et adiuvit pauperem de inopia: et posuit sicut oves familias.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Videbunt recti, et laetabuntur: et omnis iniquitas oppilabit os suum.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Quis sapiens et custodiet haec? et intelliget misericordias Domini?