< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
여호와께 감사하라! 그는 선하시며 그 인자하심이 영원함이로다
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
여호와께 구속함을 받은 자는 이같이 말할지어다 여호와께서 대적의 손에서 저희를 구속하사
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
동서 남북 각 지방에서부터 모으셨도다
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
저희가 광야 사막 길에서 방황하며 거할 성을 찾지 못하고
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
주리고 목마름으로 그 영혼이 속에서 피곤하였도다
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
이에 저희가 그 근심 중에 여호와께 부르짖으매 그 고통에서 건지시고
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
또 바른 길로 인도하사 거할 성에 이르게 하셨도다
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
여호와의 인자하심과 인생에게 행하신 기이한 일을 인하여 그를 찬송할지로다
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
저가 사모하는 영혼을 만족케 하시며 주린 영혼에게 좋은 것으로 채워주심이로다
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
사람이 흑암과 사망의 그늘에 앉으며 곤고와 쇠사슬에 매임은
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
하나님의 말씀을 거역하며 지존자의 뜻을 멸시함이라
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
그러므로 수고로 저희 마음을 낮추셨으니 저희가 엎드러져도 돕는 자가 없었도다
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
이에 저희가 그 근심 중에 여호와께 부르짖으매 그 고통에서 구원하시되
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
흑암과 사망의 그늘에서 인도하여 내시고 그 얽은 줄을 끊으셨도다
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
여호와의 인자하심과 인생에게 행하신 기이한 일을 인하여 그를 찬송할지로다
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
저가 놋문을 깨뜨리시며 쇠빗장을 꺾으셨음이로다
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
미련한 자는 저희 범과와 죄악의 연고로 곤난을 당하매
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
저희 혼이 각종 식물을 싫어하여 사망의 문에 가깝도다
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
이에 저희가 그 근심 중에서 여호와께 부르짖으매 그 고통에서 구원하시되
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
저가 그 말씀을 보내어 저희를 고치사 위경에서 건지시는도다
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
여호와의 인자하심과 인생에게 행하신 기이한 일을 인하여 그를 찬송할지로다
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
감사제를 드리며 노래하여 그 행사를 선포할지로다
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
선척을 바다에 띄우며 큰 물에서 영업하는 자는
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
여호와의 행사와 그 기사를 바다에서 보나니
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
여호와께서 명하신즉 광풍이 일어나서 바다 물결을 일으키는도다
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
저희가 하늘에 올랐다가 깊은 곳에 내리니 그 위험을 인하여 그 영혼이 녹는도다
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
저희가 이리 저리 구르며 취한 자 같이 비틀거리니 지각이 혼돈하도다
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
이에 저희가 그 근심 중에서 여호와께 부르짖으매 그 고통에서 인도하여 내시고
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
광풍을 평정히 하사 물결로 잔잔케 하시는도다
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
저희가 평온함을 인하여 기뻐하는 중에 여호와께서 저희를 소원의 항구로 인도하시는도다
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
여호와의 인자하심과 인생에게 행하신 기이한 일을 인하여 그를 찬송할지로다
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
백성의 회에서 저를 높이며 장로들의 자리에서 저를 찬송할지로다
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
여호와께서는 강을 변하여 광야가 되게 하시며 샘으로 마른 땅이되게 하시며
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
그 거민의 악을 인하여 옥토로 염밭이 되게 하시며
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
또 광야를 변하여 못이 되게 하시며 마른 땅으로 샘물이 되게 하시고
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
주린 자로 거기 거하게 하사 저희로 거할 성을 예비케 하시고
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
밭에 파종하며 포도원을 재배하여 소산을 취케 하시며
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
또 복을 주사 저희로 크게 번성케 하시고 그 가축이 감소치 않게 하실지라도
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
다시 압박과 곤란과 우환을 인하여 저희로 감소하여 비굴하게 하시는도다
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
여호와께서는 방백들에게 능욕을 부으시고 길 없는 황야에서 유리케 하시나
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
궁핍한 자는 곤란에서 높이 드시고 그 가족을 양무리 같게 하시나니
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
정직한 자는 보고 기뻐하며 모든 악인은 자기 입을 봉하리로다
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
지혜 있는 자들은 이 일에 주의하고 여호와의 인자하심을 깨달으리로다