< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
CELEBRATE il Signore; perciocchè [egli è] buono. Perciocchè la sua benignità [dura] in eterno.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
[Così] dicano quelli che sono stati riscattati dal Signore, I quali egli ha riscossi di distretta.
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
E li ha raccolti da' [diversi] paesi, Dal Levante e dal Ponente; dal Settentrione e dal mare.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Essi andavano errando per deserti, per cammini di solitudine; Non trovavano città abitata.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
[Erano] affamati ed assetati; L'anima loro spasimava in loro.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Ma, avendo gridato al Signore, mentre erano in distretta, Egli li ha tratti fuor delle loro angosce;
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
E li ha condotti per diritto cammino, Per andare in città abitata.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Celebrino [adunque] appo il Signore la sua benignità, E le sue maraviglie appo i figliuoli degli uomini.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Perciocchè egli ha saziata l'anima assetata, Ed ha empiuta di beni l'anima affamata.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
[Così dicano] quelli che dimoravano in tenebre ed in ombra di morte, Prigioni, [ritenuti] in afflizione, e ne' ferri.
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Perciocchè erano stati ribelli alle parole del Signore, Ed avevano sprezzato il consiglio dell'Altissimo;
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Onde egli aveva abbattuto il cuor loro con affanni, [Ed] erano caduti; e non [vi era] alcuno che [li] soccorresse.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Ma, avendo gridato al Signore, mentre erano in distretta, Egli li ha salvati dalle loro angosce;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
[E] li ha tratti fuor delle tenebre, e dell'ombra della morte; Ed ha rotti i lor legami.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Celebrino [adunque] appo il Signore la sua benignità, E le sue maraviglie appo i figliuoli degli uomini.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Perciocchè egli ha rotte le porte di rame, Ed ha spezzate le sbarre di ferro.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
[Così dicano] gli stolti, [ch]'erano afflitti per li lor misfatti, Ne' quali camminavano, e per le loro iniquità.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
La cui anima abbominava ogni cibo; Ed erano giunti fino alle porte della morte.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Ma, avendo gridato al Signore, mentre erano in distretta, Egli li ha salvati dalle loro angosce.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Egli ha mandata la sua parola, e li ha sanati, E liberati dalle lor malattie mortali.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Celebrino [adunque] appo il Signore la sua benignità, E le sue maraviglie appo i figliuoli degli uomini.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
E sacrifichino sacrificii di lode, E raccontino le sue opere con giubilo.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
[Così dicano] quelli che scendono nel mare sopra navi, Che fanno traffico su per le grandi acque.
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Essi veggono le opere del Signore, E le sue maraviglie nel profondo [mare].
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Perciocchè, alla sua parola, egli fa levare il vento di tempesta, Il quale alza le onde di esso.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Salgono al cielo, [poi] scendono agli abissi; L'anima loro si strugge di male.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Saltano, e traballano come un ebbro; E perdono tutto il lor senno.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Ma, gridando al Signore, mentre sono in distretta, Egli li trae fuor delle loro angosce.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Egli acqueta la tempesta, E le onde loro si fermano.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Ed essi si rallegrano che sono acquetate; Ed egli li conduce al porto da loro desiderato.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Celebrino [adunque] appo il Signore la sua benignità, E le sue maraviglie appo i figliuoli degli uomini.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Ed esaltinlo nella raunanza del popolo, E laudinlo nel concistoro degli anziani.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Egli riduce i fiumi in deserto, E le vene delle acque in luoghi aridi;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
La terra fertile in salsuggine, Per la malvagità de' suoi abitanti.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Egli riduce i deserti in guazzi d'acque. E la terra arida in vene d'acque;
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
E fa quivi abitar gli affamati, I quali [vi] fondano città da abitare.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
E seminano campi, e piantano vigne, Che producono rendita di frutto.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Ed egli li benedice, e moltiplicano grandemente; Ed egli non iscema i lor bestiami.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Poi vengono al meno, e sono abbassati Per distretta, [per] avversità, e [per] affanni.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Egli spande lo sprezzo sopra i nobili, E li fa andare errando per luoghi deserti, [ove] non [vi è] via alcuna.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
E innalza il bisognoso dalla miseria, E fa che le famiglie [moltiplicano] a guisa di gregge.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Gli [uomini] diritti, veggendo [queste cose], si rallegrano; Ma ogni iniquità si tura la bocca.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Chi [è] savio? osservi queste cose, E consideri le benignità del Signore.

< Zaburi 107 >