< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Celebrate il Signore perché è buono, perché eterna è la sua misericordia. Alleluia.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Lo dicano i riscattati del Signore, che egli liberò dalla mano del nemico
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
e radunò da tutti i paesi, dall'oriente e dall'occidente, dal settentrione e dal mezzogiorno.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Vagavano nel deserto, nella steppa, non trovavano il cammino per una città dove abitare.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Erano affamati e assetati, veniva meno la loro vita.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Nell'angoscia gridarono al Signore ed egli li liberò dalle loro angustie.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Li condusse sulla via retta, perché camminassero verso una città dove abitare.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Ringrazino il Signore per la sua misericordia, per i suoi prodigi a favore degli uomini;
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
poiché saziò il desiderio dell'assetato, e l'affamato ricolmò di beni.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Abitavano nelle tenebre e nell'ombra di morte, prigionieri della miseria e dei ceppi,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
perché si erano ribellati alla parola di Dio e avevano disprezzato il disegno dell'Altissimo.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Egli piegò il loro cuore sotto le sventure; cadevano e nessuno li aiutava.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Nell'angoscia gridarono al Signore ed egli li liberò dalle loro angustie.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Li fece uscire dalle tenebre e dall'ombra di morte e spezzò le loro catene.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Ringrazino il Signore per la sua misericordia, per i suoi prodigi a favore degli uomini;
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
perché ha infranto le porte di bronzo e ha spezzato le barre di ferro.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Stolti per la loro iniqua condotta, soffrivano per i loro misfatti;
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
rifiutavano ogni nutrimento e gia toccavano le soglie della morte.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Nell'angoscia gridarono al Signore ed egli li liberò dalle loro angustie.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Mandò la sua parola e li fece guarire, li salvò dalla distruzione.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Ringrazino il Signore per la sua misericordia e per i suoi prodigi a favore degli uomini.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Offrano a lui sacrifici di lode, narrino con giubilo le sue opere.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Coloro che solcavano il mare sulle navi e commerciavano sulle grandi acque,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
videro le opere del Signore, i suoi prodigi nel mare profondo.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Egli parlò e fece levare un vento burrascoso che sollevò i suoi flutti.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Salivano fino al cielo, scendevano negli abissi; la loro anima languiva nell'affanno.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Ondeggiavano e barcollavano come ubriachi, tutta la loro perizia era svanita.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Nell'angoscia gridarono al Signore ed egli li liberò dalle loro angustie.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Ridusse la tempesta alla calma, tacquero i flutti del mare.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Si rallegrarono nel vedere la bonaccia ed egli li condusse al porto sospirato.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Ringrazino il Signore per la sua misericordia e per i suoi prodigi a favore degli uomini.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Lo esaltino nell'assemblea del popolo, lo lodino nel consesso degli anziani.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Ridusse i fiumi a deserto, a luoghi aridi le fonti d'acqua
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
e la terra fertile a palude per la malizia dei suoi abitanti.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Ma poi cambiò il deserto in lago, e la terra arida in sorgenti d'acqua.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Là fece dimorare gli affamati ed essi fondarono una città dove abitare.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Seminarono campi e piantarono vigne, e ne raccolsero frutti abbondanti.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Li benedisse e si moltiplicarono, non lasciò diminuire il loro bestiame.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Ma poi, ridotti a pochi, furono abbattuti, perché oppressi dalle sventure e dal dolore.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Colui che getta il disprezzo sui potenti, li fece vagare in un deserto senza strade.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Ma risollevò il povero dalla miseria e rese le famiglie numerose come greggi.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Vedono i giusti e ne gioiscono e ogni iniquo chiude la sua bocca.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Chi è saggio osservi queste cose e comprenderà la bontà del Signore.

< Zaburi 107 >