< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
»Danket dem HERRN, denn er ist freundlich, ja, ewiglich währt seine Gnade«:
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
so sollen die vom HERRN Erlösten sprechen, die er befreit hat aus Drangsal
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
und die er gesammelt aus den Ländern vom Aufgang her und vom Niedergang, vom Norden her und vom Meer.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Sie irrten umher in der Wüste, der Öde, und fanden den Weg nicht zu einer Wohnstatt;
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
gequält vom Hunger und vom Durst, wollte ihre Seele in ihnen verschmachten.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
und leitete sie auf richtigem Wege, daß sie kamen zu einer bewohnten Ortschaft: –
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern,
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
daß er die lechzende Seele gesättigt und die hungernde Seele gefüllt hat mit Labung.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Die da saßen in Finsternis und Todesnacht, gefangen in Elend und Eisenbanden –
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
denn sie hatten Gottes Geboten getrotzt und den Ratschluß des Höchsten verachtet,
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
so daß er ihren Sinn durch Leiden beugte, daß sie niedersanken und keinen Helfer hatten –;
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
er führte sie heraus aus Finsternis und Todesnacht und zersprengte ihre Fesseln: –
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern,
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
daß er eherne Türen zerbrochen und eiserne Riegel zerschlagen.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Die da krank waren infolge ihres Sündenlebens und wegen ihrer Verfehlungen leiden mußten –
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
vor jeglicher Speise hatten sie Widerwillen, so daß sie den Pforten des Todes nahe waren –;
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten;
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
er sandte sein Wort, sie gesund zu machen, und ließ sie aus ihren Gruben entrinnen: –
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern;
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
sie mögen Opfer des Dankes bringen und seine Taten mit Jubel verkünden!
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Die aufs Meer gefahren waren in Schiffen, auf weiten Fluten Handelsgeschäfte trieben,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
die haben das Walten des HERRN geschaut und seine Wundertaten auf hoher See.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Denn er gebot und ließ einen Sturm entstehn, der hoch die Wogen des Meeres türmte:
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
sie stiegen empor zum Himmel und fuhren hinab in die Tiefen, so daß ihr Herz vor Angst verzagte;
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
sie wurden schwindlig und schwankten wie Trunkne, und mit all ihrer Weisheit war’s zu Ende: –
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er befreite sie aus ihren Ängsten;
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
er stillte das Ungewitter zum Säuseln, und das Toben der Wogen verstummte;
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
da wurden sie froh, daß es still geworden, und er führte sie zum ersehnten Hafen: –
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern;
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
sie mögen ihn erheben in der Volksgemeinde und im Kreise der Alten ihn preisen!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Er wandelte Ströme zur Wüste und Wasserquellen zu dürrem Land,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
fruchtbares Erdreich zu salziger Steppe wegen der Bosheit seiner Bewohner.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Wiederum machte er wüstes Land zum Wasserteich und dürres Gebiet zu Wasserquellen
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
und ließ dort Hungrige seßhaft werden, so daß sie eine Stadt zum Wohnsitz bauten
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
und Felder besäten und Weinberge pflanzten, die reichen Ertrag an Früchten brachten;
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
und er segnete sie, daß sie stark sich mehrten, und ließ ihres Viehs nicht wenig sein.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Dann aber nahmen sie ab und wurden gebeugt durch den Druck des Unglücks und Kummers;
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
»über Edle goß er Verachtung aus und ließ sie irren in pfadloser Öde«.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Den Armen aber hob er empor aus dem Elend und machte seine Geschlechter wie Kleinviehherden.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
»Die Gerechten sehen’s und freuen sich, alle Bosheit aber muß schließen ihren Mund«.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Wer ist weise? Der beachte dies und lerne die Gnadenerweise des HERRN verstehn!

< Zaburi 107 >