< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
"Dem Herrn sagt Dank! Denn er ist gut. Auf ewig währet seine Huld."
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
So singen die vom Herrn Erlösten, die er aus Feindes Hand befreit
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
und aus den Ländern sammelt von Morgen, Abend, Mitternacht und Süden. -
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Sie irren in der Steppenwüste und finden keine Bahn zur Wohnstatt hin.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Sie leiden Durst und Hunger, und ihre Seele sinkt darob in Ohnmacht.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Sie schreien zu dem Herrn in ihrer Not; Er rettet sie aus ihren Ängsten
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
und leitet sie auf rechtem Wege, die Wohnstatt zu erreichen.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
daß er ihr Lechzen stillt und ihren Hunger mit dem Nötigen befriedigt! -
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
In Finsternis und Todesschatten sitzen sie, gebannt in Elend und in Eisen;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
denn Gottes Worten widerspenstig, verschmähen sie des Höchsten Rat.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Durch Mühsal beugt er ihren Sinn; sie werden machtlos; niemand hilft.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Sie schrein zum Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Aus Finsternis und Todesschatten führt er sie, und ihre Fesseln sprengt er auf.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
daß er zertrümmert eherne Pforten und Eisenriegel bricht! -
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Die Kranken leiden schwer ob ihres Sündenwandels und wegen ihrer Missetaten,
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
daß sie vor jeder Speise ekelt und sie des Todes Pforten schon berühren.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Sie schreien zu dem Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Er schickt sein Wort, macht sie gesund und rettet sie vor ihren Grüften.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
ihm Dankesopfer bringen, jubelnd seine Taten künden! -
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Die auf der See in Schiffen fahren und ihr Geschäft auf großen Wassern treiben,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
erblicken hier des Herren Werke und seine Wunder mit der tiefen Flut.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Ein Sturm erhebt sich auf sein Wort, und seine Wellen türmen sich.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Sie steigen bis zum Himmel, fahren in die Tiefen. Ihr Leben ist gefährdet.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Sie tanzen, schwanken wie Betrunkene. Dahin ist ihre ganze Kunst.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Sie schrein zum Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Er macht den Sturm zum Säuselwind; da legen sich des Meeres Wellen.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Sie jubeln, daß sie stille liegen und er sie an ihr Endziel führt.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
und ihn vor allem Volk erheben und ihn im Kreis der Alten loben! -
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Er macht zur Wüste Ströme, zu dürrem Lande Quellenorte,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
ein fruchtbar Land zum salzigen Grund, der Bosheit der Bewohner wegen.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Er macht zum Wasserteich die Wüste und dürres Land zum Quellenort;
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
die Hungrigen läßt er hier wohnen; Sie bauen eine Wohnstatt dort,
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
besäen Felder, pflanzen Weinberge, die lohnend Früchte tragen.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Er segnet sie, daß sie sich riesig mehren, und läßt ihr Vieh sich nicht vermindern.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Vermindern sie sich, werden sie gebeugt von Druck und Elend und von Jammer,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
dann gießt auf Fürsten er Verachtung aus und führt sie in die unwegsame Öde.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Doch aus dem Elend hebt er Arme auf und macht Geschlechter Herden gleich.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Das sehen Redliche und freuen sich, und jeder Frevelmund verstummt. -
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Wer weise ist, beachtet dies, und Anerkennung finden so des Herren Gnadentaten.