< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Louez l'Éternel, car Il est bon, car sa miséricorde est éternelle!
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Qu'ainsi parlent les rachetés de l'Éternel, qu'il a rachetés des mains de l'ennemi,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
et recueillis de tout pays, du Levant et du Couchant, du Septentrion et de la mer.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Ils furent errants au désert, dans une voie solitaire, et ils ne trouvaient pas une ville où habiter;
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
ils éprouvaient la faim et la soif; leur âme en eux était défaillante.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et ils crièrent à l'Éternel dans leur détresse, et Il les délivra de leurs perplexités,
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
et leur fit prendre la voie directe pour arriver à une ville où pouvoir habiter.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils rendent grâces à l'Éternel de sa miséricorde, et disent ses merveilles aux enfants des hommes!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Car Il a satisfait l'âme altérée, et comblé de biens l'âme affamée.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Ceux qui habitaient les ténèbres et l'ombre de la mort, prisonniers de la misère et des fers…
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Car ils résistèrent aux paroles de Dieu, et méprisèrent les décrets du Très-haut.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Aussi courba-t-Il leur cœur sous la peine; ils succombèrent, et ne furent point assistés.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Mais ils crièrent à l'Éternel dans leur détresse, et Il les délivra de leurs perplexités;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Il les tira des ténèbres et de l'ombre de la mort, et rompit leurs fers.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils rendent grâces à l'Éternel de sa miséricorde, et disent ses merveilles aux enfants des hommes!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Car Il a brisé les portes d'airain, et mis en pièces les verrous de fer.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Les insensés qui suivaient la voie de la révolte, et à cause de leurs crimes se virent humiliés…
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Toute nourriture excitait leur dégoût, et ils arrivaient aux portes de la mort.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Mais ils crièrent à l'Éternel dans leur détresse, et Il les délivra de leurs perplexités;
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Il émit sa parole, et les guérit, et les retira de leurs tombeaux.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils rendent grâces à l'Éternel de sa miséricorde, et disent ses merveilles aux enfants des hommes!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Qu'ils Lui offrent les sacrifices de la reconnaissance, et publient ses hauts faits avec des cris de joie!
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Ceux qui se mirent en mer sur des navires, et firent la manœuvre sur les grandes eaux,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
furent témoins des œuvres de Dieu, et des merveilles qu'il opère dans les flots.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Il dit, et excita un vent de tempête, qui souleva les vagues de la mer;
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
elles montèrent vers le ciel, descendirent dans l'abîme, leur âme dans le danger était éperdue;
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
saisis du vertige, ils chancelaient, comme étant ivres, et toute leur sagesse était évanouie.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Mais ils crièrent à l'Éternel dans leur détresse, et Il les délivra de leurs perplexités,
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Il fit cesser la tourmente qui devint silencieuse, et les vagues se turent;
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
et ils furent joyeux, quand elles se calmèrent, et Il les conduisit au port désiré.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils rendent grâces à l'Éternel de sa miséricorde, et disent ses merveilles aux enfants des hommes!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Qu'ils L'exaltent dans l'assemblée du peuple, et Le louent dans la séance des anciens!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Il change les fleuves en désert, et les sources des eaux en sol aride,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
la plaine fertile en steppe salée, à cause de la méchanceté de ses habitants.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Il change le désert en une masse d'eaux, et la terre desséchée en sources d'eaux,
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
et Il y établit ceux qui sont affamés, et là ils fondent des villes, pour les habiter.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Ils ensemencent des champs, et plantent des vignes qui donnent leurs fruits pour revenu.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Et Il les bénit, et ils deviennent très nombreux, et Il n'amoindrit pas leurs bestiaux.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Or ils étaient amoindris et accablés par l'oppression, le malheur et les peines;
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
c'est lui qui verse le mépris sur les princes, et Il les fait errer dans un désert sans chemin;
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
mais Il relève le pauvre de sa misère, et rend les familles égales à des troupeaux.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
C'est ce que voient les hommes droits, et ils se réjouissent, et tous les méchants ont la bouche fermée.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Que tout homme sage prenne garde à ceci, et soit attentif aux grâces de l'Éternel!

< Zaburi 107 >