< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Célébrez l'Éternel, car il est bon, car sa miséricorde demeure à toujours!
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Qu'ainsi disent les rachetés de l'Éternel, ceux qu'il a rachetés de la main de l'oppresseur,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Et qu'il a rassemblés des pays d'orient et d'occident, de l'aquilon et du midi.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Ils erraient par le désert, dans un chemin solitaire; ils ne trouvaient point de ville habitable.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Ils étaient affamés et altérés; leur âme défaillait en eux.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Il les a conduits par le droit chemin, pour arriver à une ville habitable.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Car il a rassasié l'âme altérée, et rempli de biens l'âme affamée.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Ceux qui habitaient les ténèbres et l'ombre de la mort, retenus dans l'affliction et dans les fers,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Pour avoir été rebelles aux paroles de Dieu, et avoir méprisé le conseil du Très-Haut;
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Il avait humilié leur cœur par la souffrance; ils succombaient loin de tout secours.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Il les a tirés des ténèbres et de l'ombre de la mort; il a rompu leurs liens.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Car il a brisé les portes d'airain, et rompu les barreaux de fer.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Les insensés qui étaient affligés à cause de la voie de leurs trangressions et de leurs iniquités;
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Leur âme avait en horreur toute nourriture; ils touchaient aux portes de la mort.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Il a envoyé sa parole, et il les a guéris, et les a retirés de leurs tombeaux.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Qu'ils offrent des sacrifices d'actions de grâces, et racontent ses œuvres en chantant de joie!
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Ceux qui descendent sur la mer dans des navires, et qui trafiquent sur les grandes eaux,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Ceux-là ont vu les œuvres de l'Éternel, et ses merveilles dans les lieux profonds.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Il parla, et fit lever un vent de tempête, qui souleva les vagues de la mer.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Ils montent aux cieux; ils descendent aux abîmes; leur âme se fond d'angoisse.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Ils tournoient et chancellent comme un homme ivre; toute leur sagesse leur manque.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse, et il les a retirés de leurs angoisses.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Il arrête la tempête, la changeant en calme, et les ondes se taisent.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Ils se réjouissent de ce qu'elles sont calmées; et il les conduit au port qu'ils désiraient.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils célèbrent la bonté de l'Éternel, et ses merveilles envers les fils des hommes!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Qu'ils l'exaltent dans l'assemblée du peuple; qu'ils le louent dans le conseil des anciens!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Il change les fleuves en désert, et les sources d'eaux en un sol aride;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
La terre fertile en lande salée, à cause de la méchanceté de ses habitants.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Il change le désert en étang, et la terre aride en sources d'eaux.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Il y fait habiter ceux qui étaient affamés; et ils fondent une ville pour l'habiter.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Ils ensemencent des champs et plantent des vignes, qui rendent du fruit tous les ans.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Il les bénit, et ils se multiplient extrêmement; il ne laisse point diminuer leur bétail.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Puis, ils sont amoindris et humiliés par l'oppression, le malheur et la souffrance.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Il répand le mépris sur les grands, et les fait errer dans un désert sans chemin.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Mais il relève le pauvre de l'affliction, et rend les familles nombreuses comme des troupeaux.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Les hommes droits le voient et s'en réjouissent; mais tous les injustes ont la bouche fermée.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Que celui qui est sage prenne garde à ces choses, et considère les bontés de l'Éternel.

< Zaburi 107 >