< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Alléluiah! Rendez gloire au Seigneur, parce qu'il est bon, parce que sa miséricorde est éternelle.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Qu'ainsi disent ceux qui ont été rachetés par le Seigneur, qu'il a délivrés de la main de leurs ennemis et rassemblés des contrées
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Du levant et du couchant, de la mer et de l'aquilon.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Ils ont erré dans le désert sans eau; ils n'y ont point trouvé le chemin d'une cité habitable,
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Et ils avaient faim, ils avaient soif; et leur âme était défaillante.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et, dans leur tribulation, ils crièrent au Seigneur, et il les retira de leur détresse.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Et il les conduisit dans le droit chemin, afin qu'ils arrivassent à une cité habitable.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils rendent gloire à la miséricorde du Seigneur et à ses prodiges en faveur des fils des hommes;
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Car il a rassasié leur âme vide, et rempli de biens leur âme affamée.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Assis dans les ténèbres et à l'ombre de la mort, ils étaient enchaînés par la pauvreté et le fer;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Parce qu'ils avaient provoqué les voix du Seigneur, et avaient irrité le conseil du Très-Haut.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Et leur cœur fut humilié dans leurs labeurs, et ils furent sans force, et nul n'était là pour les secourir.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et dans leurs tribulations ils crièrent au Seigneur, et il les retira de leur détresse.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Et il les tira des ténèbres et de l'ombre de la mort, et brisa leurs chaînes.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Car il a fait voler en éclats les portes d'airain; il a brisé les verrous de fer.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Il les a aidés à sortir de la voie de leur iniquité; et, à cause de leurs infidélités, ils avaient été humiliés.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Leur âme avait pris en abomination tout aliment, et déjà ils étaient près des portes de la mort.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Et dans leurs tribulations ils crièrent au Seigneur, et il les sauva de leur détresse.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Et il envoya sa parole, et il les a guéris, et il les arrachés de leur perdition.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Et qu'ils lui offrent des oblations de louanges, et qu'ils annoncent ses œuvres avec des transports d'allégresse.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Ceux qui voguent sur la mer dans leurs barques, et qui trafiquent au milieu des eaux,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Ceux-là ont vu les œuvres du Seigneur, et ses merveilles dans l'abîme.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Il dit, et le vent impétueux de la tempête s'est levé, et les vagues ont bondi.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Elles montent jusqu'aux cieux et descendent jusqu'aux abîmes, et l'âme des matelots succombe à la violence du mal.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Ils sont troublés, ils chancellent comme des hommes ivres, et toute leur sagesse a été engloutie.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Et dans leur tribulation ils ont crié au Seigneur, et il les a retirés de leur détresse.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Et il a commandé à la tempête, et elle s'est changée en une brise légère, et les flots ont fait silence.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Et les hommes se sont réjouis de leur calme, et le Seigneur les a conduits au port désiré.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Qu'ils l'exaltent dans l'assemblée du peuple, et le louent sur le siège des anciens.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Il a changé des fleuves en un désert, et des eaux jaillissantes en une terre altérée;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Et une terre fertile en un lieu saumâtre, à cause de la malice de ceux qui l'habitaient.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Il a fait d'un désert un étang plein d'eau, et d'une terre sans eau des vallons arrosés.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Et il y a mis des affamés, et ils ont bâti des cités habitables.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Et ils ont ensemencé des champs, et ils ont planté des vignes, et ils en ont récolté les produits.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Et il les a bénis, et ils se sont prodigieusement multipliés, et il n'a pas amoindri le nombre de leur bétail.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Puis ils ont déchu, et ils ont été maltraités par les tribulations, les maux et la douleur.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Et le mépris s'est répandu sur leurs princes, et Dieu les a laissés s'égarer en des lieux impraticables et sans voie.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Et il a délivré le pauvre de sa misère, et il a traité sa famille comme des brebis.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Les justes le verront et en seront réjouis, et toute iniquité fermera sa bouche.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Quel est le sage qui gardera ces choses, et comprendra les miséricordes du Seigneur?