< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Célébrez Yahweh, car il est bon, car sa miséricorde est éternelle.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Qu'ainsi disent les rachetés de Yahweh, ceux qu'il a rachetés des mains de l'ennemi,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
et qu'il a rassemblés de tous les pays, de l'orient et de l'occident, du nord et de la mer!
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Ils erraient dans le désert, dans un chemin solitaire, sans trouver une ville à habiter.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
En proie à la faim, à la soif, ils sentaient leur âme défaillir.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Dans leur détresse, ils crièrent vers Yahweh, et il les délivra de leurs angoisses.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Il les mena par le droit chemin, pour les faire arriver à une ville habitable.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils louent Yahweh pour sa bonté, et pour ses merveilles en faveur du fils de l'homme.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Car il a désaltéré l'âme altérée, et comblé de biens l'âme affamée.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Ils habitaient les ténèbres et l'ombre de la mort, prisonniers dans la souffrance et dans les fers.
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Parce qu'ils s'étaient révoltés contre les oracles du Dieu, et qu'ils avaient méprisé le conseil du Très-Haut,
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
il humilia leur cœur par la souffrance; ils s'affaissèrent, et personne ne les secourut.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Dans leur détresse, ils crièrent vers Yahweh, et il les sauva de leurs angoisses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Il les tira des ténèbres et de l'ombre de la mort, et il brisa leurs chaînes.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Qu'ils louent Yahweh pour sa bonté, et pour ses merveilles en faveur des fils de l'homme.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Car il a brisé les portes d'airain et mis en pièces les verrous de fer.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Les insensés! par leur conduite criminelle, et par leurs iniquités, ils avaient attiré sur eux la souffrance.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Leur âme avait en horreur toute nourriture, et ils touchaient aux portes de la mort.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Dans leur détresse, ils crièrent vers Yahweh, et il les sauva de leurs angoisses.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Il envoya sa parole et il les guérit, et il les fit échapper de leurs tombeaux.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils louent Yahweh pour sa bonté, et pour ses merveilles en faveur des fils de l'homme!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Qu'ils offrent des sacrifices d'actions de grâce, et qu'ils publient ses œuvres avec des cris de joie!
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Ils étaient descendus sur la mer dans des navires, pour faire le négoce sur les vastes eaux:
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
— ceux là ont vu les œuvres de Yahweh, et ses merveilles au milieu de l'abîme —
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Il dit, et il fit lever un vent de tempête, qui souleva les flots de la mer.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Ils montaient jusqu'aux cieux, ils descendaient dans les abîmes; leur âme défaillait dans la peine.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Saisis de vertige, ils chancelaient comme un homme ivre, et toute leur sagesse était anéantie.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Dans leur détresse, ils crièrent vers Yahweh, et il les tira de leurs angoisses.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Il changea l'ouragan en brise légère, et les vagues de la mer se turent.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Ils se réjouirent en les voyant apaisées, et Yahweh les conduisit au port désiré.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Qu'ils louent Yahweh pour sa bonté, et pour ses merveilles en faveur des fils de l'homme!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Qu'ils l'exaltent dans l'assemblée du peuple, et qu'ils le célèbrent dans le conseil des anciens!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Il a changé les fleuves en désert, et les sources d'eau en sol aride;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Le pays fertile en plaine de sel, à cause de la méchanceté de ses habitants.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Il a fait du désert un bassin d'eau, et de la terre aride un sol plein de sources.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Il y établit les affamés, et ils fondèrent une ville pour l'habiter.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Ils ensemencèrent des champs, et ils plantèrent des vignes, et ils recueillirent d'abondantes récoltes.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Il les bénit, et ils se multiplièrent beaucoup, et il ne laissa pas diminuer leurs troupeaux.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Ils avaient été réduits à un petit nombre et humiliés, sous l'accablement du malheur et de la souffrance.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Il avait répandu la honte sur leurs princes, il les avait fait errer dans des déserts sans chemins.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Mais il a relevé le malheureux de la misère, et il a rendu les familles pareilles à des troupeaux.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Les hommes droits le voient et se réjouissent, et tous les méchants ferment la bouche.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Que celui qui est sage prenne garde à ces choses, et qu'il comprenne les bontés de Yahweh!

< Zaburi 107 >