< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
'Give ye thanks to Jehovah, For good, for to the age [is] His kindness:'
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let the redeemed of Jehovah say, Whom He redeemed from the hand of an adversary.
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And from the lands hath gathered them, From east and from west, From north, and from the sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered in a wilderness, in a desert by the way, A city of habitation they have not found.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry — yea — thirsty, Their soul in them becometh feeble,
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cry unto Jehovah in their adversity, From their distress He delivereth them,
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And causeth them to tread in a right way, To go unto a city of habitation.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
They confess to Jehovah His kindness, And His wonders to the sons of men.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For He hath satisfied a longing soul, And a hungry soul hath filled [with] goodness.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Inhabitants of dark places and death-shade, Prisoners of affliction and of iron,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they changed the saying of God, And the counsel of the Most High despised.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
And He humbleth with labour their heart, They have been feeble, and there is no helper.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cry unto Jehovah in their adversity, From their distresses He saveth them.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He bringeth them out from the dark place, And death-shade, And their bands He draweth away.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
They confess to Jehovah His kindness, And His wonders to the sons of men.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For He hath broken doors of brass, And bars of iron He hath cut.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools, by means of their transgression, And by their iniquities, afflict themselves.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
All food doth their soul abominate, And they come nigh unto the gates of death,
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And cry unto Jehovah in their adversity, From their distresses He saveth them,
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sendeth His word and healeth them, And delivereth from their destructions.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
They confess to Jehovah His kindness, And His wonders to the sons of men,
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And they sacrifice sacrifices of thanksgiving, And recount His works with singing.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Those going down [to] the sea in ships, Doing business in many waters,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
They have seen the works of Jehovah, And His wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
And He saith, and appointeth a tempest, And it lifteth up its billows,
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They go up [to] the heavens, they go down [to] the depths, Their soul in evil is melted.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reel to and fro, and move as a drunkard, And all their wisdom is swallowed up.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
And they cry to Jehovah in their adversity, And from their distresses He bringeth them out.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He establisheth a whirlwind to a calm, And hushed are their billows.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
And they rejoice because they are quiet, And He leadeth them to the haven of their desire.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
They confess to Jehovah His kindness, And His wonders to the sons of men,
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
And they exalt Him in the assembly of the people, And in the seat of the elders praise Him.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He maketh rivers become a wilderness, And fountains of waters become dry land.
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A fruitful land becometh a barren place, For the wickedness of its inhabitants.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He maketh a wilderness become a pool of water, And a dry land become fountains of waters.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And He causeth the hungry to dwell there, And they prepare a city of habitation.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And they sow fields, and plant vineyards, And they make fruits of increase.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
And He blesseth them, and they multiply exceedingly, And their cattle He doth not diminish.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
And they are diminished, and bow down, By restraint, evil, and sorrow.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He is pouring contempt upon nobles, And causeth them to wander in vacancy — no way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
And setteth on high the needy from affliction, And placeth families as a flock.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright do see and rejoice, And all perversity hath shut her mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Who [is] wise, and observeth these? They understand the kind acts of Jehovah!

< Zaburi 107 >