< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
O give thanks to the LORD, for [he is] good; for his mercy [endureth] for ever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let the redeemed of the LORD say [so], whom he hath redeemed from the hand of the enemy;
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And gathered them out of the lands, from the east, and from the west, from the north, and from the south.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered in the wilderness in a solitary way; they found no city to dwell in.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry and thirsty, their soul fainted in them.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the LORD in their trouble, [and] he delivered them out of their distresses.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And he led them forth by the right way, that they might go to a city of habitation.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Oh that [men] would praise the LORD [for] his goodness, and [for] his wonderful works to the children of men!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he satisfieth the longing soul, and filleth the hungry soul with goodness.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Such as sit in darkness and in the shades of death, [being] bound in affliction and iron;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they rebelled against the words of God, and contemned the counsel of the Most High:
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Therefore he brought down their heart with labor; they fell down, and [there was] none to help.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the LORD in their trouble, [and] he saved them out of their distresses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought them out of darkness and the shades of death, and broke their bands asunder.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Oh that [men] would praise the LORD [for] his goodness, and [for] his wonderful works to the children of men!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he hath broken the gates of brass, and cut the bars of iron asunder.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools, because of their transgression, and because of their iniquities, are afflicted.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Their soul abhorreth all manner of food; and they draw near to the gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cry to the LORD in their trouble, he saveth them out of their distresses.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent his word, and healed them, and delivered [them] from their destructions.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Oh that [men] would praise the LORD [for] his goodness, and [for] his wonderful works to the children of men!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And let them sacrifice the sacrifices of thanksgiving, and declare his works with rejoicing.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
They that go down to the sea in ships, that do business on great waters;
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
These see the works of the LORD, and his wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For he commandeth, and raiseth the stormy wind, which lifteth up its waves.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They mount up to the heaven, they go down again to the depths: their soul is melted because of trouble.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reel to and fro, and stagger like a drunken man, and are at their wit's end.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they cry to the LORD in their trouble, and he bringeth them out of their distresses.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He maketh the storm a calm, so that the waves [of the sea] are still.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Then are they glad because they are quiet; so he bringeth them to their desired haven.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Oh that [men] would praise the LORD [for] his goodness, and [for] his wonderful works to the children of men!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them exalt him also in the congregation of the people, and praise him in the assembly of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He turneth rivers into a wilderness, and the water-springs into dry ground;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A fruitful land into barrenness, for the wickedness of them that dwell in it.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He turneth the wilderness into a standing water, and dry ground into water-springs.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And there he maketh the hungry to dwell, that they may prepare a city for habitation;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And sow the fields, and plant vineyards, which may yield fruits of increase.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He blesseth them also, so that they are multiplied greatly; and suffereth not their cattle to decrease.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Again, they are diminished and brought low through oppression, affliction, and sorrow.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He poureth contempt upon princes, and causeth them to wander in the wilderness, [where there is] no way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Yet he setteth the poor on high from affliction, and maketh him families like a flock.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The righteous shall see [it], and rejoice: and all iniquity shall stop her mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Whoever [is] wise, and will observe these [things], even they shall understand the loving-kindness of the LORD.

< Zaburi 107 >