< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Give thanks to Yahweh for [he is] good for [is] for ever covenant loyalty his.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let them say [the] redeemed of Yahweh whom he has redeemed them from [the] hand of [the] opponent.
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And from [the] lands he has gathered them from east and from west from north and from [the] sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered about in the wilderness in a desolate place of a way a city of dwelling not they found.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry also thirsty life their in them it was fainting away.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to Yahweh when it was distress to them from troubles their he delivered them.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And he led them by a way straight to go to a city of dwelling.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks to Yahweh covenant loyalty his and wonders his to [the] children of humankind.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he satisfies a throat longing and a throat hungry he fills good thing[s].
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
[those who] sat of Darkness and deep darkness prisoners of affliction and iron.
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
For they had rebelled against [the] words of God and [the] counsel of [the] Most High they had spurned.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
And he humbled with trouble heart their they stumbled and there not [was] a helper.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to Yahweh when it was distress to them from troubles their he saved them.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought out them from darkness and deep darkness and fetters their he tore apart.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks to Yahweh covenant loyalty his and wonders his to [the] children of humankind.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he breaks down gates of bronze and bars of iron he cuts down.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools from [the] way of transgression their and from iniquities their they were afflicted.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
All food it loathed throat their and they reached to [the] gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to Yahweh when it was distress to them from troubles their he saved them.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent word his and he healed them and he may deliver [them] (from pits their. *LAH(b)*)
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks to Yahweh covenant loyalty his and wonders his to [the] children of (humankind. *LAH(b)*)
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And let them sacrifice sacrifices of thanksgiving and let them recount works his (with a shout of joy. *L(abh)*)
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
[those who] went down the Sea in ships [those who] did business on [the] waters (many. *L(abh)*)
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
They they saw [the] works of Yahweh and wonders his (in [the] deep. *L(abh)*)
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
And he spoke and he appointed a wind of a storm and it lifted up (waves its. *L(abh)*)
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They went up [the] heavens they went down [the] deeps soul their in distress (it melted. *LB(ah)*)
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They staggered and they may trembled like drunkard and all skill their (it was confused. *LB(ah)*)
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
And they cried out to Yahweh when it was distress to them and from troubles their he brought out them.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He raised [the] storm into a calm and they were still waves their.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
And they rejoiced for they were quiet and he guided them to [the] harbor of desire their.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks to Yahweh covenant loyalty his and wonders his to [the] children of humankind.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
And let them exalt him in [the] assembly of [the] people and in [the] seat of [the] elders let them praise him.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He made rivers into a wilderness and springs of water into thirsty ground.
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A land of fruit into saltiness from [the] evil of [those who] dwell in it.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He made a wilderness into a pool of water and a land dry into springs of water.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And he caused to dwell there hungry [people] and they established a city of dwelling.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And they sowed fields and they planted vineyards and they produced fruit of produce.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
And he blessed them and they multiplied exceedingly and cattle their not he made few.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
And they became few and they were bowed down from [the] pressure of calamity (and sorrow. *L(abh)*)
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
[he was] pouring out Contempt on noble [people] and he made wander them in a wasteland not a way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
And he set on high [the] needy from affliction and he made like flock families.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
They see upright [people] so they may rejoice and all unrighteousness it shuts mouth its.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Who? [is] wise and let him observe these [things] and let them consider carefully [the] covenant loyalti of Yahweh.

< Zaburi 107 >