< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Give thanks to the Lord for his goodness for his kindness endures forever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let this be the song of the ransomed, whom the Lord has redeemed from distress,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
gathering them from all lands, east, west, north, and south.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
In the wastes of the desert some wandered, finding no way to a city inhabited.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Full of hunger and thirst, their spirit failed.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses,
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
guiding them straight on the way, till they reached an inhabited city.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them thank the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people;
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
for the thirsty he satisfies, and the hungry he fills with good things.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Some sat in darkness and gloom prisoners in irons and misery,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
for rebelling against God’s word, and spurning the Most High’s counsel.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Their heart was bowed with toil; there was no one to help when they stumbled.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Out of darkness and gloom he brought them, and burst their chains.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them praise the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he shattered the gates of bronze, and broke bars of iron.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Some were sick from their wicked ways, and suffering because of their sins.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
All manner of food they hated; they had come to the gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent his word and healed them, and delivered their life from the pit.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them praise the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Let them offer to him thankofferings, and with joy tell what things he has done.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Some crossed the sea in ships, doing business in great waters.
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
They have seen what the Lord can do, and his wonderful deeds on the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
At his command rose a tempest, which lifted the waves on high.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Up to heaven they went, down to the depths; their courage failed them.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They staggered and reeled like drunkards; all their skills useless.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He stilled the storm to a whisper, and the waves of the sea were hushed.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
They were glad, because it was quiet; they were led to the haven they longed for.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them praise the Lord, for his kindness, for his wonderful deeds for people.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Where the people assemble, extol him, and praise him in council of elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He turns streams into a wilderness, springs of water into thirsty land,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
fruitful land into a salt waste, because of the sin of the people.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
A desert he makes pools of water, a land of drought into springs of water.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
He settles the hungry therein, they establish a city to live in.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
They sow fields and plant vineyards, which furnish a fruitful yield.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
By his blessing they multiply greatly, and he lets not their cattle decrease.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Yet when they are bowed and diminished by oppression, misfortune, or sorrow,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
he pours contempt upon princes, and on trackless wastes leads them astray
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
He lifts the poor out of misery, and makes families fruitful as flocks.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
At this sight shall the upright be glad, and all wicked mouths shall be stopped.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Let those who are wise observe this, and consider the love of the Lord

< Zaburi 107 >