< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
BOOK FIFTH: Oh give thanks unto the Lord; for he is good; for unto eternity endureth his kindness.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Thus let the Lord's redeemed say, even those whom he hath redeemed from the hand of the adversary;
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And whom he hath gathered out of the [various] lands, from the east, and from the west, from the north, and from the sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered about in the wilderness, in the desert path; they could not find an inhabited city:
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry and thirsty, their soul within them fainted.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried unto the Lord when they were in distress, [and] out of their afflictions he delivered them.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And he led them forth on the right way, that they might go to an inhabited city.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
They [therefore] shall give thanks unto the Lord for his kindness, and [proclaim] his wonders to the children of men!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he satisfied the longing soul, and the hungry soul he filled with good.—
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Such as sit in darkness and in the shadow of death, bound in misery and [fetters of] iron; —
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they have rebelled against the words of God, and have contemned the counsel of the Most High;
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
And he humbled with trouble their heart; they stumbled, and there was none to help;
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
But when they cry unto the Lord when they are in distress, he saveth them out of their afflictions;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He bringeth them out of darkness and the shadow of death, and teareth their bands asunder.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
They [therefore] shall give thanks unto the Lord for his kindness, and [proclaim] his wonders to the children of men!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he hath broken the doors of copper, and the bolts of iron hath he hewn asunder.—
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools, because of their transgression, and because of their iniquities, are afflicted.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
All manner of food their soul abhorreth; and they draw near unto the gates of death;
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
But when they cry unto the Lord when they are in distress, he saveth them out of their afflictions.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sendeth his word and healeth them, and delivereth them from their graves.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
They [therefore] shall give thanks unto the Lord for his kindness, and [proclaim] his wonders to the children of men!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
They shall also sacrifice the sacrifices of thanksgiving, and relate his deeds with joyful song.—
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
They who go down to the sea in ships, who do business on great waters; —
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
These have seen the works of the Lord, and his wonders on the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For he spoke, and he raised the stormy wind, which lifteth up its waves.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They would mount up to heaven, they would go down to the depths: their soul was melted because of their danger.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They would reel to and fro, and stagger like a drunken man, and all their wisdom was exhausted.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
And they cried unto the Lord when they were in distress, and he brought them out of their afflictions.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He calmed the storm into a whisper, and stilled were the waves of the sea.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
And they were rejoiced because they were silent: and then he guided them unto their desired haven.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
They [therefore] shall give thanks unto the Lord for his kindness, and [proclaim] his wonders to the children of men!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
And they must exalt him in the congregation of the people, and in the assembly of the elders must they praise him.—
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He changeth rivers into a wilderness, and water-springs into parched ground;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A fruitful land into a salty waste, for the wickedness of those that dwell therein.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He changeth the wilderness into a pool of water, and desert land into water-springs.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And there he causeth to dwell the hungry, that they may found an inhabited city;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And they sow fields, and plant vineyards, that they may yield the fruits of the [annual] product.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He also blesseth them, and they multiply greatly, and he suffereth not their cattle to diminish.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
They were also diminished and bowed low through oppression, misfortune, and sorrow:
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He [then] poureth contempt upon princes, and causeth them to wander in a pathless wilderness.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
And he exalteth the needy from misery, and maketh [his] families like flocks.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The righteous shall see it, and rejoice; but all wickedness shall stop her mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Whoever is wise, let him observe these things, and let [all] understand the kindness of the Lord.