< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
BOOK V 'O give thanks unto the LORD, for He is good, for His mercy endureth for ever.'
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
So let the redeemed of the LORD say, whom He hath redeemed from the hand of the adversary;
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And gathered them out of the lands, from the east and from the west, from the north and from the sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered in the wilderness in a desert way; they found no city of habitation.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry and thirsty, their soul fainted in them.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried unto the LORD in their trouble, and He delivered them out of their distresses.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And He led them by a straight way, that they might go to a city of habitation.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks unto the LORD for His mercy, and for His wonderful works to the children of men!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For He hath satisfied the longing soul, and the hungry soul He hath filled with good.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Such as sat in darkness and in the shadow of death, being bound in affliction and iron —
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they rebelled against the words of God, and contemned the counsel of the Most High.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Therefore He humbled their heart with travail, they stumbled, and there was none to help —
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
They cried unto the LORD in their trouble, and He saved them out of their distresses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought them out of darkness and the shadow of death, and broke their bands in sunder.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks unto the LORD for His mercy, and for His wonderful works to the children of men!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For He hath broken the gates of brass, and cut the bars of iron in sunder.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Crazed because of the way of their transgression, and afflicted because of their iniquities —
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Their soul abhorred all manner of food, and they drew near unto the gates of death —
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
They cried unto the LORD in their trouble, and He saved them out of their distresses;
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent His word, and healed them, and delivered them from their graves.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks unto the LORD for His mercy, and for His wonderful works to the children of men!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And let them offer the sacrifices of thanksgiving, and declare His works with singing.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
They that go down to the sea in ships, that do business in great waters —
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
These saw the works of the LORD, and His wonders in the deep;
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For He commanded, and raised the stormy wind, which lifted up the waves thereof;
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They mounted up to the heaven, they went down to the deeps; their soul melted away because of trouble;
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reeled to and fro, and staggered like a drunken man, and all their wisdom was swallowed up —
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
They cried unto the LORD in their trouble, and He brought them out of their distresses.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He made the storm a calm, so that the waves thereof were still.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Then were they glad because they were quiet, and He led them unto their desired haven.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks unto the LORD for His mercy, and for His wonderful works to the children of men!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them exalt Him also in the assembly of the people, and praise Him in the seat of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He turneth rivers into a wilderness, and watersprings into a thirsty ground;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A fruitful land into a salt waste, for the wickedness of them that dwell therein.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He turneth a wilderness into a pool of water, and a dry land into watersprings.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And there He maketh the hungry to dwell, and they establish a city of habitation;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And sow fields, and plant vineyards, which yield fruits of increase.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He blesseth them also, so that they are multiplied greatly, and suffereth not their cattle to decrease.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Again, they are minished and dwindle away through oppression of evil and sorrow.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He poureth contempt upon princes, and causeth them to wander in the waste, where there is no way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Yet setteth He the needy on high from affliction, and maketh his families like a flock.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright see it, and are glad; and all iniquity stoppeth her mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Whoso is wise, let him observe these things, and let them consider the mercies of the LORD.

< Zaburi 107 >