< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Give ye thanks unto Jehovah; for he is good; for his loving-kindness [endureth] for ever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let the redeemed of Jehovah say so, whom he hath redeemed from the hand of the oppressor,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And gathered out of the countries, from the east and from the west, from the north and from the sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered in the wilderness in a desert way, they found no city of habitation;
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry and thirsty, their soul fainted in them:
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried unto Jehovah in their trouble, [and] he delivered them out of their distresses,
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And he led them forth by a right way, that they might go to a city of habitation.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks unto Jehovah for his loving-kindness, and for his wondrous works to the children of men;
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he hath satisfied the longing soul and filled the hungry soul with good.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Such as inhabit darkness and the shadow of death, bound in affliction and iron,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they had rebelled against the words of God, and had despised the counsel of the Most High; ...
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
And he bowed down their heart with labour; they stumbled, and there was none to help:
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried unto Jehovah in their trouble, [and] he saved them out of their distresses;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought them out of darkness and the shadow of death, and broke their bands in sunder.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks unto Jehovah for his loving-kindness, and for his wondrous works to the children of men;
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he hath broken the gates of bronze, and cut asunder the bars of iron.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools, because of their way of transgression, and because of their iniquities, are afflicted;
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Their soul abhorreth all manner of food, and they draw near unto the gates of death:
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cry unto Jehovah in their trouble, [and] he saveth them out of their distresses;
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sendeth his word, and healeth them, and delivereth them from their destructions.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks unto Jehovah for his loving-kindness, and for his wondrous works to the children of men,
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And let them offer the sacrifices of thanksgiving, and declare his works in joyful song.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
They that go down to the sea in ships, that do business in great waters,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
These see the works of Jehovah, and his wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For he speaketh, and raiseth the stormy wind, which lifteth up the waves thereof:
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They mount up to the heavens, they go down to the depths; their soul is melted because of trouble;
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reel to and fro, and stagger like a drunken man, and they are at their wits' end:
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they cry unto Jehovah in their trouble, and he bringeth them out of their distresses;
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He maketh the storm a calm, and the waves thereof are still:
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
And they rejoice because they are quiet; and he bringeth them unto their desired haven.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks unto Jehovah for his loving-kindness, and for his wondrous works to the children of men;
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them exalt him also in the congregation of the people, and praise him in the session of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He maketh rivers into a wilderness, and water-springs into dry ground;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
A fruitful land into a plain of salt, for the wickedness of them that dwell therein.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He maketh the wilderness into a pool of water, and the dry land into water-springs;
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And there he maketh the hungry to dwell, and they establish a city of habitation;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And sow fields, and plant vineyards, which yield fruits of increase;
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
And he blesseth them, so that they are multiplied greatly; and he suffereth not their cattle to decrease.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
And they are diminished and brought low, through oppression, adversity, and sorrow:
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He poureth contempt upon nobles, and causeth them to wander in a pathless waste;
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
But he secureth the needy one on high from affliction, and maketh [him] families like flocks.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright shall see it, and rejoice; and all unrighteousness shall stop its mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Whoso is wise, let him observe these things, and let them understand the loving-kindnesses of Jehovah.