< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Alleluia. Confess to the Lord, for he is good, for his mercy is with every generation.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let those who have been redeemed by the Lord say so: those whom he redeemed from the hand of the enemy and gathered from the regions,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
from the rising of the sun and its setting, from the north and from the sea.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered into solitude in a waterless place. They did not find the way of the city to be their dwelling place.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
They were hungry, and they were thirsty. Their soul fainted within them.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to the Lord in tribulation, and he rescued them in their necessity.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
And he led them in the right way, so that they might go forth to a city of habitation.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let his mercies confess to the Lord, and let his miracles confess to the sons of men.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he has satisfied the empty soul, and he has satisfied the hungry soul with good things:
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
those sitting in darkness and in the shadow of death, shackled by extreme poverty and by iron.
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
For they exasperated the eloquence of God, and they irritated the deliberation of the Most High.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
And their heart was brought low with hardships. They were weakened, and there was no one to help them.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to the Lord in their tribulation, and he freed them from their distress.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
And he led them out of darkness and the shadow of death, and he broke apart their chains.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let his mercies confess to the Lord, and let his miracles confess to the sons of men.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he has crushed the gates of brass and broken the iron bars.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
He has taken them up, from the way of their iniquity. For they were brought low, because of their injustices.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Their soul abhorred all food, and they drew near even to the gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
And they cried out to the Lord in their tribulation, and he delivered them in their necessity.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent his word, and he healed them, and he rescued them from their utter destruction.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let his mercies confess to the Lord, and let his miracles confess to the sons of men.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
And let them offer sacrifice with the sacrifice of praise, and let them announce his works in exultation.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Those who descend to the sea in ships, making their livelihood in the great waters:
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
these have seen the works of the Lord and his wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
He spoke: and a windstorm stood up, and its waves were exalted.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They ascend even to the heavens, and they descend even to the abyss. Their soul will waste away in distress.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They were troubled, and they moved like a drunkard, and all their wisdom was consumed.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
And they cried out to the Lord in their tribulation, and he led them out of their distress.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
And he replaced the storm with a breeze, and its waves were stilled.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
And they were joyful that it was stilled, and he led them into the haven that they desired.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let his mercies confess to the Lord, and let his miracles confess to the sons of men.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
And let them exalt him in the Church of the people, and praise him in the chair of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He has placed rivers in the desert and sources of water in dry places,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
a fruit-bearing land in the midst of brine, before the malice of those who dwell in it.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He has placed a desert in the midst of pools of waters, and a land without water in the midst of sources of water.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And he has gathered the hungry together there, and they constructed a city of habitation.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And they sowed fields and planted vineyards, and they produced the fruit of nativity.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
And he blessed them, and they were multiplied exceedingly. And he did not diminish their beasts of burden.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
And they became few, and they were afflicted by the tribulation of evils and of sorrow.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Contempt was poured over their leaders, and he caused them to wander in an impassable place, and not on the way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
And he helped the poor out of destitution, and he stationed families like sheep.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright will see, and they will rejoice. And every iniquity will block its mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Who is wise and will keep these things? And who will understand the mercies of the Lord?