< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
O give praise to the Lord, for he is good: for his mercy is unchanging for ever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let those whose cause the Lord has taken up say so, his people whom he has taken out of the hands of their haters;
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Making them come together out of all the lands, from the east and from the west, from the north and from the south.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They were wandering in the waste places; they saw no way to a resting-place.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Their souls became feeble for need of food and drink.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they sent up their cry to the Lord in their sorrow, and he gave them salvation out of all their troubles;
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Guiding them in the right way, so that they might come into the town of their resting-place.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let men give praise to the Lord for his mercy, and for the wonders which he does for the children of men!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
He gives its desire to the unresting soul, so that it is full of good things.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Those who were in the dark, in the black night, in chains of sorrow and iron;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Because they went against the words of God, and gave no thought to the laws of the Most High:
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
So that he made their hearts weighted down with grief; they were falling, and had no helper.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they sent up their cry to the Lord in their sorrow, and he gave them salvation out of all their troubles.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He took them out of the dark and the black night, and all their chains were broken.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let men give praise to the Lord for his mercy, and for the wonders which he does for the children of men!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
The doors of brass are broken by his arm, and the bands of iron are cut in two.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Foolish men, because of their sins, and because of their wrongdoing, are troubled;
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
They are disgusted by all food, and they come near to the doors of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they send up their cry to the Lord in their sorrow, and he gives them salvation out of all their troubles.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent his word and made them well, and kept them safe from the underworld.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let men give praise to the Lord for his mercy, and for the wonders which he does for the children of men!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Let them make offerings of praise, giving news of his works with cries of joy.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Those who go down to the sea in ships, who do business in the great waters;
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
They see the works of the Lord, and his wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For at his word comes up the storm-wind, lifting high the waves.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
The sailors go up to heaven, and down into the deep; their souls are wasted because of their trouble.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They are turned here and there, rolling like a man who is full of wine; and all their wisdom comes to nothing.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they send up their cry to the Lord in their sorrow, and he gives them salvation out of all their troubles.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He makes the storm into a calm, so that the waves are at peace.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Then they are glad, because the sea is quiet, and he takes them to the harbour of their desire.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let men give praise to the Lord for his mercy, and for the wonders which he does for the children of men!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them give glory to him in the meeting of the people, and praise among the chiefs.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He makes rivers into waste places, and springs of water into a dry land;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
He makes a fertile country into a salt waste, because of the sins of those who are living there.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He makes a waste land into a place of water, and a dry land into water-springs.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
And there he gives the poor a resting-place, so that they may make themselves a town;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
And put seed in the fields and make vine-gardens, to give them fruit.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He gives them his blessing so that they are increased greatly, and their cattle do not become less.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
And when they are made low, and crushed by trouble and sorrow,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He puts an end to the pride of kings, and sends them wandering in the waste lands where there is no way.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
But he puts the poor man on high from his troubles, and gives him families like a flock.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright see it and are glad: the mouth of the sinner is stopped.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Let the wise give thought to these things, and see the mercies of the Lord.

< Zaburi 107 >