< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let the redeemed of the LORD say so, whom He has redeemed from the hand of the enemy
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
and gathered from the lands, from east and west, from north and south.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Some wandered in desert wastelands, finding no path to a city in which to dwell.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
They were hungry and thirsty; their soul fainted within them.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried out to the LORD in their trouble, and He delivered them from their distress.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
He led them on a straight path to reach a city where they could live.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks to the LORD for His loving devotion and His wonders to the sons of men.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For He satisfies the thirsty and fills the hungry with good things.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Some sat in darkness and in the shadow of death, prisoners in affliction and chains,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
because they rebelled against the words of God and despised the counsel of the Most High.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
He humbled their hearts with hard labor; they stumbled, and there was no one to help.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried out to the LORD in their trouble, and He saved them from their distress.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought them out of darkness and the shadow of death and broke away their chains.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them give thanks to the LORD for His loving devotion and His wonders to the sons of men.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For He has broken down the gates of bronze and cut through the bars of iron.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools, in their rebellious ways, and through their iniquities, suffered affliction.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
They loathed all food and drew near to the gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried out to the LORD in their trouble, and He saved them from their distress.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent forth His word and healed them; He rescued them from the Pit.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks to the LORD for His loving devotion and His wonders to the sons of men.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Let them offer sacrifices of thanksgiving and declare His works with rejoicing.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Others went out to sea in ships, conducting trade on the mighty waters.
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
They saw the works of the LORD, and His wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For He spoke and raised a tempest that lifted the waves of the sea.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They mounted up to the heavens, then sunk to the depths; their courage melted in their anguish.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reeled and staggered like drunkards, and all their skill was useless.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they cried out to the LORD in their trouble, and He brought them out of their distress.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He calmed the storm to a whisper, and the waves of the sea were hushed.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
They rejoiced in the silence, and He guided them to the harbor they desired.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them give thanks to the LORD for His loving devotion and His wonders to the sons of men.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them exalt Him in the assembly of the people and praise Him in the council of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He turns rivers into deserts, springs of water into thirsty ground,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
and fruitful land into fields of salt, because of the wickedness of its dwellers.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He turns a desert into pools of water and a dry land into flowing springs.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
He causes the hungry to settle there, that they may establish a city in which to dwell.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
They sow fields and plant vineyards that yield a fruitful harvest.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He blesses them, and they multiply greatly; He does not let their herds diminish.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
When they are decreased and humbled by oppression, evil, and sorrow,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He pours out contempt on the nobles and makes them wander in a trackless wasteland.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
But He lifts the needy from affliction and increases their families like flocks.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright see and rejoice, and all iniquity shuts its mouth.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Let him who is wise pay heed to these things and consider the loving devotion of the LORD.

< Zaburi 107 >