< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Halleluja! Lov HERREN, thi han er god, thi hans Miskundhed varer evindelig!
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Saa skal HERRENS genløste sige, de, han løste af Fjendens Haand
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
og samlede ind fra Landene, fra Øst og Vest, fra Nord og fra Havet.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
I den øde Ørk for de vild, fandt ikke Vej til beboet By,
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
de led baade Sult og Tørst, deres Sjæl var ved at vansmægte;
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
men de raabte til HERREN i Nøden, han frelste dem af deres Trængsler
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
og førte dem ad rette Vej, saa de kom til beboet By.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Lad dem takke HERREN for hans Miskundhed, for hans Underværker mod Menneskens Børn.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Thi han mætted den vansmægtende Sjæl og fyldte den sultne med godt.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
De sad i Mulm og Mørke, bundne i Pine og Jern,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
fordi de havde staaet Guds Ord imod og ringeagtet den Højestes Raad.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Deres Hjerte var knuget af Kummer, de faldt, der var ingen, som hjalp;
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
men de raabte til HERREN i Nøden, han frelste dem af deres Trængsler,
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
førte dem ud af Mørket og Mulmet og sønderrev deres Baand.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Lad dem takke HERREN for hans Miskundhed, for hans Underværker mod Menneskens Børn.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Thi han sprængte Døre af Kobber og sønderslog Slaaer af Jern.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
De sygnede hen for Synd og led for Brødes Skyld,
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
de væmmedes ved al Slags Mad, de kom Dødens Porte nær;
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
men de raabte til HERREN i Nøden, han frelste dem af deres Trængsler,
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
sendte sit Ord og lægede dem og frelste deres Liv fra Graven.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Lad dem takke HERREN for hans Miskundhed, for hans Underværker mod Menneskens Børn
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
og ofre Lovprisningsofre og med Jubel forkynde hans Gerninger.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
De for ud paa Havet i Skibe, drev Handel paa vældige Vande,
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
blev Vidne til HERRENS Gerninger, hans Underværker i Dybet;
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
han bød, og et Stormvejr rejste sig, Bølgerne taarnedes op;
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
mod Himlen steg de, i Dybet sank de, i Ulykken svandt deres Mod;
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
de tumled og raved som drukne, borte var al deres Visdom;
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
men de raabte til HERREN i Nøden, han frelste dem af deres Trængsler,
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
skiftede Stormen til Stille, saa Havets Bølger tav;
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
og glade blev de, fordi det stilned; han førte dem til Havnen, de søgte.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Lad dem takke HERREN for hans Miskundhed, for hans Underværker mod Menneskens Børn,
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
ophøje ham i Folkets Forsamling og prise ham i de Ældstes Kreds!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Floder gør han til Ørken og Kilder til øde Land,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
til Saltsteppe frugtbart Land for Ondskabens Skyld hos dem, som bor der.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Ørken gør han til Vanddrag, det tørre Land til Kilder;
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
der lader han sultne bo, saa de grunder en By at bo i,
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
tilsaar Marker og planter Vin og høster Afgrødens Frugt.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Han velsigner dem, de bliver mange, han lader det ikke skorte paa Kvæg.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
De bliver faa og segner under Modgangs og Kummers Tryk,
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
han udøser Haan over Fyrster og lader dem rave i vejløst Øde.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Men han løfter den fattige op af hans Nød og gør deres Slægter som Hjorde;
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
de oprigtige ser det og glædes, men al Ondskab lukker sin Mund.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Hvo som er viis, han mærke sig det og lægge sig HERRENS Naade paa Sinde!

< Zaburi 107 >