< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Hvalite Jahvu jer je dobar, jer je dovijeka ljubav njegova!
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Tako nek' reknu svi otkupljenici koje Jahve otkupi iz ruke dušmanske
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
i koje skupi iz svih zemalja, s istoka i sa zapada, sa sjevera i s juga.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Lutahu pustinjom, u samoći pustoj, puta ne nalazeć' do naseljena grada.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Gladni su bili, žeđu izmoreni, duša je klonula u njima.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi, i on ih istrže iz svih nevolja.
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Pravim ih putem pÓovede da stignu ka gradu naseljenu.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Jer gladnu dušu on nasiti, dušu izgladnjelu on napuni dobrima.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
U mraku sjeđahu i u tmini, sputani bijedom i gvožđima,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
jer su prkosili besjedama Božjim i prezreli naum Svevišnjega.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Srce im stoga skrši patnjama: posrtahu, a ne bješe nikog da im pomogne.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Izvede ih iz tmina i mraka, raskide okove njihove.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Jer razbi vrata mjedena i gvozdene polomi zasune.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Zbog svojih bezakonja bolovahu oni, ispaštajuć' svoje opačine:
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
svako se jelo gadilo duši njihovoj, do vrata smrti oni dođoše.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Riječ svoju posla da ih ozdravi i život im spasi od jame grobne.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Nek' prinose žrtve zahvalnice i kličući nek' djela njegova kazuju!
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Oni koji lađama zaploviše morem da po vodama silnim trguju:
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
oni vidješe djela Jahvina, čudesa njegova na pučini.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
On reče i olujni se vjetar uzvitla što u visinu diže valove mora.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Do neba se dizahu, u bezdan se spuštahu, u nevolji duša im ginula.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Teturahu i posrtahu kao pijani, sva ih je mudrost izdala.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Smiri oluju u tih povjetarac, valovi morski umukoše.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Obradovaše se tišini, u željenu luku on ih povede.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Neka ga uzvisuju u narodnom zboru, neka ga hvale u vijeću staraca!
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
On pretvori rijeke u pustinju, a izvore vodene u žednu zemlju;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
plodonosnu zemlju u slanu pustaru zbog zloće žitelja njezinih.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
On obrati pustinju u jezero, a zemlju suhu u vodene izvore
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
i naseli ondje izgladnjele te podigoše grad gdje će živjeti.
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Zasijaše njive, posadiše vinograde što im doniješe obilnu ljetinu.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
I on ih blagoslovi te se namnožiše silno i stada im se ne smanjiše.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Prorijeđeni bjehu i prezreni pod teretom patnja i nevolja.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
Onaj što izlijeva prezir na knezove pusti ih da po bespuću pustom lutaju.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Iz nevolje pÓodiže ubogog i obitelji k'o stada ÓumnožÄi.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Videć' to, čestiti neka se raduju, a zloća neka sebi usta začepi!
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Tko je mudar nek' o svemu tom razmišlja i nek' uvidi dobrotu Jahvinu!

< Zaburi 107 >